
Habari Digital
@HabariDigital_ • 245,570 subscribers
Kwa Habari, Burudani na Matukio, Kitaifa na Kimataifa, Saa Ishirini na Nne, Siku Saba za Wiki.
Shorts
Videos

Papa Leo XIV ameonekana kupuuza na kuikwepa bendera inayowakilisha jumuiya za watu wenye mwelekeo tofauti wa kijinsia wakiwemo wale wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja. Papa Leo XIV ameonyesha dalili za kukataa jumuiya hizo wakati akisalimiana na kubariki hadhara iliyojitoleza wakati akizungumza na wataaluma wa habari siku ya Jumatatu Mei 12, 2025, kwenye Ukumbi wa Paul VI mjini Vatican. Hata hivyo baadhi wa watu wanatoa maoni juu ya video hiyo na kueleza kuwa Papa Leo hakupuuza bendera hiyo bali hakuwa na uwezo wa kusalimia pande zote mbili (kushoto na kulia) wakati akikatiza katikati hadhara hiyo, hivyo alilazimika kusalimia kila upande kwa zamu huku akisonga mbele, na alipofika eneo lenye bendera ilikuwa ni zamu ya upande wa kulia huku bendera ikiwa upande wa kushoto. Wanaharakati na taasisi mbalimbali zinazounga mkono jumuiya hizo, tayari wameanza kumtuhumu na kumkosoa Papa Leo XIV kwa kupuuza bendera hiyo. Nini maoni yako.....
Habari Digital83,956 次观看 • 1 年前

VIDEO: Aliyekuwa Naibu Rais Kenya, Rigathi Gachagua amelazimika kutoka mbio kunusuru usalama wake, baada ya kundi la vijana kuzua vurugu hivyo kulazimu ibada ya mazishi kukatishwa, Tukio hilo limetokea katika eneo la Limuru, kaunti ya Kiambu ambapo magari ya msafara wa Gachagua yameharibiwa huku baadhi wa wasaidizi wake wakijeruhiwa. Wasaidizi wa Gachagua wanaituhumu serikali kuhusika na mpango huo, wakidai njama hiyo ilipangwa na Mbunge wa Limuru ambaye naye amekana kuhusika na vurugu hizo. #HabariDigital 🎥KTN
Habari Digital97,047 次观看 • 1 年前

VIDEO: Kufuatia matukio ya utekaji na mauaji yanayoripotiwa kutokea nchini., Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu, amezitaka mamlaka kualika wataalamu kutoka nje ya Tanzania kwaajili ya kuvichunguza vyombo vya ulinzi na usalama. Lissu ameyasema hayo leo Septemba 11, 2024 alipowasili Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam akitokea nchini Ubelgiji.
Habari Digital106,480 次观看 • 1 年前

VIDEO: Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Godbless Lema [ Godbless E.J. Lema ] ametoa utabiri wake baada ya kufutwa usajili wa kanisa la ufufuo na uzima linaloongozwa na askofu Josephat Gwajima. Aidha Lema amekosoa hatua zilizochukuliwa na mamlaka akieleza kuwa aliyetakiwa kuchukuliwa hatua ni askofu Gwajima na si kuifungia taasisi yote.
Habari Digital61,250 次观看 • 1 年前

VIDEO: Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu amesema atakwenda mahakamani kuishitaki serikali ya Tanzania. Lissu amesisitiza kuwa atashinda kesi hiyo hivyo serikali ya Tanzania itatakiwa kumlipa fidia na wasipofanya hivyo basi ataanza kuzikamata ndege za Tanzania zinazofanya safari zake nje ya nchi
Habari Digital81,733 次观看 • 1 年前

VIDEO: Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amedai kuwa siasa na dini havipaswi kutenganishwa huku akitoa mifano kadhaa ikiwemo kuuawa kwa Kiongozi Mkuu wa Iran Ayatollah Ali Khamenei, katazo la kutoka nje yalipotokea maandamano ya Oktoba, 2025, na kuongeza mfano wa uongozi wa kisiasa na kidini wa Papa Leo XIV, Vatican.
Habari Digital22,467 次观看 • 4 个月前

VIDEO: Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Jakaya Kikwete ameitaka Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kushughulikia malalamiko ya maadili dhidi ya viongozi wa umma akiwemo yeye mwenyewe, kisha kuwajulisha wananchi ukweli dhidi ya malalamiko hayo.
Habari Digital32,445 次观看 • 7 个月前