MwanzoTvPlus's banner
MwanzoTvPlus's profile picture

MwanzoTvPlus

@MwanzoTvPlus124,244 subscribers

Independent Online Media serving East Africa with premier news - Uncensored and Undaunted

Videos

MwanzoTvPlus's profile picture

#TANZANIA: CHADEMA KUANZISHA KAMPENI NZITO KUSHINIKIZA LISSU KUACHIWA HURU, "TUTAANDAA MAANDAMANO MAKUBWA, HATUTAPIGA MAGOTI" Makamu Mwenyekiti wa Chadema Tanzania Bara, John Heche leo Aprili 09, 2026 wakati wa mjadala maalum ulioendeshwa kwa njia ya mtandao ambapo Tundu Antiphas Lissu anatimiza mwaka mmoja (siku 365) akiwa gerezani ametoa wito kwa Watanzania walio ndani na nje ya nchi hususani Vijana kuanzisha kampeni maalum ya kuzishinikiza Mamlaka kumuachia huru Mwenyekiti wa Chama hicho, Tundu Lissu akisema Lissu hajatenda kosa bali amebambikiwa kesi. “Jambo langu kwako wewe Kijana unayetuona, unayedai kwamba unatuunga mkono sio kusemea chinichini, tunapaswa kuanzisha kampeni kubwa wamuachie Tundu Lissu kwasababu Lissu amekamatwa kwa ajili yetu, kwasababu wote tunajua na wote tunaamini Lissu hana kosa, ni Mtu mwema anayetupigania, ili asikate tamaa ili asiwe na baridi kule aliko anafikiri kwamba nimekamatwa na Watu niliokuwa nawapigania wamerudi nyuma, tunapaswa kuanzisha kuanzia leo kampeni kubwa kwenye kila platform Instagram, Facebook, TikTok, Twitter ya kumdai Tundu Lissu” - Heche “Watu wetu wa Diaspora mfanye kama waliofanya Watu wa Diaspora waliokuwepo wa Afrika Kusini wakati ule , Vijana wetu mlioko ndani ya nchi tuandike vipeperushi visambae kwenye masoko, kwenye nguzo za umeme zikiwa na picha ya Lissu na ujumbe wa kutaka Lissu aachiwe” - John Heche, Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara. Zaidi:

MwanzoTvPlus

39,542 просмотров • 3 месяцев назад