
Webiro Wakazi Wassira #TheLeader
@Wakazi • 255,007 subscribers
Artist | Activist | Actor | Hip Hop Connoisseur | Content Creator | Politician | Workethic | 1/4 of SSK | [email protected] | Link: https://t.co/QgttN8fCtU
Shorts
Videos

BONGOSTAR SEARCH: HII HAPANA Hatuwezi kukuza VIPAJI VIPYA kama tutakuwa tunavi HUMILIATE, MISTREAT & UNDERMINE kwa this type of unfair judging & condescending approach. Huyu Binti anaimba, rap, na ni bilingual mwenye personality na exposure ya ulaya. Hizo ni Taarifa ambazo amezitoa ndani ya sekunde 20 za mwanzo; zilitosha kwa yeye kupewa BENEFIT OF DOUBT, na hata namna ya ku-engage nae ingeweza kuwa friendlier na yenye way more entertaining content than kum-shutdown hivi! IKUMBUKWE; Washiriki ni AMATEURS na WAKO NERVOUS. Unaweza kuwa INDIFFERENT & UNBIASED as a JUDGE ila sio kuwa CRUEL; you can KILL THEIR CONFIDENCE na hata kama anajua akafanya BAD PERFORMANCE. Ndio maana WAZOEFU humfanya Mshiriki a-relax, kumsifia alivyovaa, kumuuliza nini anaimba, kum-wish goodluck, ili a calm down kabla ya kuperform. MFANO mimi kama Judge, ningemtania kuhusu BRITISH ACCENT yake, au ningemuuliza LONDON alikuwa anafanya nini, etc. Way BETTER CONTENT for THE AUDIENCE. Alafu disqualification yake ni kuwa SAUTI IKO CHINI, Really? Hicho si ni kielelezo tosha kuwa SHE IS NERVOUS? 🤷🏾♂️ Mimi nimemsikia kuimba anajua (hajakosea kitu), na angeruhusiwa 5-7 more seconds ambapo wimbo ulikuwa unaenda ku-TRANSITION, ndio tungejua uwezo wake zaidi. Na hivyo hivyo kwenye ku-rap, ame-rhyme, ameflow na amekaa kwenye pocket; Mashairi yake kweli ni Explicit ila sio kiiivyo. Hata kina SIMON COWELL, wakiona RAW POTENTIAL, ila iko nervous, huwa wanasimamisha encourage them, then wanawapa second chance, na sio kuwa dismiss. Na mtu wa hivyo DEVELOPMENT & GROWTH ARC yake inaenda as anaendelea kuwepo kwenye Shindano na pia inawapa Audience nafasi ya ku-fall in love with Washiriki. Mimi, WAKAZI, as a former judge wa UNITALENT SHOW, huyo dada ANAJUA KUIMBA; anaimba kwa Mix ya “HEAD & CHEST VOICE” na LOWER REGISTER MEZZO ALTO ndio her VOICE TYPE. ANAWEZA KU-RAP pia na Content yake inashabihiana na Female Rappers wa kisasa (Meg The Stallion, Sexy Red, Latto) so hiyo VERSATILITY yake ni golden. Ana PERSONALITY and Particular SENSE OF FASHION with GOOD COMMUNICATION SKILLS (English & Swahili). Na hizo zote ndio QUALITIES ZA KUTENGENEZA A STAR. You can do better… The Leader
Webiro Wakazi Wassira #TheLeader140,515 просмотров • 1 месяц назад

LACK OF EXPOSURE INAWA EXPOSE WATAWALA HARAMU Yaani Rais KILAZA, Aliyeandika Speech KILAZA, Mshauri wake (wa kumwambia atumie issue ya Mafuta as topic) ni KILAZA, Aliyepenyeza “Kimemo” (sijui ni Usalama Wa Taifa au Msaidizi au GIRISHONI) nae KILAZA!! 😫☹️ Unafanyaje DIRECT COMPARISON ya bei za Mafuta, na Nchi ambazo zina PURCHASING POWER PARITY ya matrillioni, na pia kuna CURRENCY DISPARITY ya 1:2600 (U$D), 1:3000 (Euro) and even 1:20 (KTsh) ?! Marekani state maskini kuliko zote mshahara kima cha chini ni $8 kwa Saa ($64 kwa siku) na jimbo hilo mafuta ni $3 kwa Gallon (so kwa liter ni $0.75 au Tsh 1875). Mshahara Wa Maskini wa Siku wa 160,000, na Mafuta lita 1875. Wewe Daktari unamlipa laki 9 kwa mwezi (yaani 30,000 kwa siku) alafu unajisifia kumuuzia mafuta kwa Tsh 3800 🤷🏾♂️ Alafu unatoa takwimu za Uongo, na anayekusahihisha nae anatudanganya pia. Mmeharibu THAMANI YA HELA yetu, kiasi kwamba senti hazina thamani. Marekani ukiona 8.00 sio mia nane, bali ni dola 8; hizo sifuri ni za SENTI!! Pia hamjui tofauti ya METRIC SYSTEM (Litre, Kilo, Meter, Centimeter) na IMPERIAL SYSTEM (Ounce, Gallon, Pound, Inches). MSIGWA anakuja kutwambia bei ya Mafuta kwa Tani.. Kitu cha UJAZO anapima UZITO. Kazi ya Viongozi ni kuleta ahueni kwa Wananchi, ila nyie HARAMU tunajua mpo kwa maslahi yenu binafsi ndio maana unatetea kutopunguza kodi kwa hoja na takwimu za mtu ambae hajaenda shule, hana exposure, na anayepiga Siasa/Propaganda. Tokeni hapa… HAMUWEZI KUTUDANGANYA, MTAJUTA KUTUSOMESHA! The Leader
Webiro Wakazi Wassira #TheLeader57,935 просмотров • 2 месяцев назад

Don’t Kill the Messenger…. Rafiki yangu Rachel ana ujumbe huu kwa Waumini wa Kanisa la Gwajima na Walinzi wake There’s an alleged issued manhunt for Askofu Gwajima, led by the infamous Mafwele Everyone who has been critical of SERIKALI HARAMU, please take precautions. SAFETY!
Webiro Wakazi Wassira #TheLeader34,469 просмотров • 2 месяцев назад

HADIDU ZA REJEA: MAMA WA KAMBO ANAJIZIMA DATA Tumeshakubaliana kuwa yeye ni “Illegimate President”, na pia Tume yake ni ILLEGITIMATE: ina CONFLICT OF INTEREST, pia yeye sio Legit hivyo hana mamlaka kisheria kuunda Tume. Anatakiwa a STEP DOWN, asubiri TUME ZA KIMATAIFA zilizoafikiwa na WANANCHI zifanye kazi. BUT for argument sake, tufanye ni sawa Tume ndio hiyo. Kweli hizo ndio TERMS OF REFERENCE (Hadidu za Rejea) za kufanyia uchunguzi wa “Kilichotokea”?! Nani kamwambia Tunachunguza VURUGU sisi? Hujui Sababu za Raia (Maana sio Vijana tu) kuandamana? Kweli Watu wamepigwa risasi wewe unataka kuchunguza NGOs? WATU WAMELIPWA? Jamani waliofanya Fundraiser si ni CCM na wakapata karibia BILLION 100 za michango. Mmeandika ILANI ambayo haijui Malalamiko ya Wananchi, alafu unashangaa why HATUWATAKI Familia ya Deusdetius Soka inahitaji Kulipwa Kuandamana? Familia ya Marehemu Ali Kibao Inahitaji kulipwa Kuandamana? Waumini Wa Gwajima walioporwa Haki ya Kuabudu wanahitaji Kulipwa Kuandamana? Wananchi milioni 6 waliompigia Kura Tundu Lissu mwaka 2020 walioona anapewa KESI YA UHAINI kisa amedai Reforms, wanahitaji Kulipwa kuandamana? Wafuasi wa Luhaga Mpina walioshuhudia anakatwa kama Mgombea, wanahitaji kulipwa Kuandamana? Vijana waliosoma na Wasio na Ajira na Wenye Njaa, ambao wameshuhudia Vigogo na Watoto wao wanavyofuja Mali za Taifa lao, wanahitaji kulipwa Kuandamana? Wafuasi wa Polepole wanahitaji Kulipwa Kuandamana? Familia na Mashabiki wa Roma Mkatoliki, Sativa, Tito Magoti, Eric Kabendera, Abdul Nondo, etc wanahitaji kulipwa kuandamana? STOP INSULTING OUR INTELLIGENCE!! Sasa hiyo ni Tume ya Uchunguzi kweli? Mbona ni kama Mmeshafanya Uchunguzi wenu na Mnawapa Maelekezo ya nini wafanye!! Sisi tunataka TUME HURU ZA KIMATAIFA zichunguze WIZI WA UCHAGUZI, na MAUAJI YA HALAIKI YA VYOMBO VYA DOLA. Kama kutakuwa na wajumbe wa Ndani basi Wawe ambao Wanachi tutawaafiki (wasio na INTEREST nor ULTERIOR MOTIVES) Najua Mnajizima Data maana wenyewe mnanusa mwisho wenu, ila kazi itafanyika hata offline… The Leader
Webiro Wakazi Wassira #TheLeader83,733 просмотров • 7 месяцев назад

FANYENI REHEARSAL KAMA MNATAKA KUIMBA LIVE…!! Otherwise, just accept kubakia “studio artists” tu. Badala ya kuwekeza kwenye nguo, magari, mabodyguard, fake chains & fake views, hebu; • Fanyeni rehearsal 1-2 weekly, hata kama hamna show. • Mkienda gym fanyeni Cardio badala ya weightlifting • Lipeni WAPIGA BENDI vizuri, na hela unazitunzwa wape kama Bonus • Fanya rehearsal na bendi sio unawapa nyimbo wewe hutokei • Sikiliza mawazo ya wapiga bendi, kuwa nao kitu kimoja na sio ujione wewe unawaamrisha tu • Study show za wakali wengine, ujifunze some techniques za kuboresha show yako • Kwenye rehearsal, fanya kila kitu ambacho unatarajia kufanya kwenye show. Kama uta dance, basi dance pia huku una practice • Train your breath control, ukifanya cardio uwe unaimba pia ili ujue maeneo yaku pause, na kujifunza pacing (kulingana na performance time) • Sahau kuhusu “Hit Song” yako. Unapofanya live, technically ni kama unafanya kitu kipya. So mambo ya kuimba neno alafu unanyamaza mashabiki wamalizie, linakufanya huonekane huwezi live… IMBA • Tambua audience; sio kila hadhira iko familiar na nyimbo zako hata kama ziliwahi ku-hit… mfano awards za kimataifa zinaangaliwa na watu ambao sio mashabiki wako, na pia wanaangalia kupitia TV. Sasa wewe ukiwa unanyamaza eti mashabiki waitikie, potential new fans wanaona hujui au umesahau mistari huku kwenye TV. • Ukitaka kuimba ki superstar kwa kunyamaza nyamaza, basi kuwa na strong BVs (Back Vocalists) ambao ume practice nao vya kutosha Mwenye masikio na asikie! Dancers, Mataa, Nguo, Moshi au Cheche za stage hazitoweza kukuokoa wala kuficha udhaifu wako The Leader.
Webiro Wakazi Wassira #TheLeader128,545 просмотров • 1 год назад

MSIGWA KAISHIWA PAWA PRESS HAIELEWEKI; umeita LOCAL MEDIA kuongelea INTERNATIONAL MEDIA, alafu unalilia WATALII, kisha unaanza PROPAGANDA. Hii ni Dalili KUELEKEA KIBLA. Unataka Media zifanye kazi kwa “Uwazi, Haki na Uwajibikaji”? Michael Jackson aliimba, STARTING WITH MAN ON THE MIRROR, akimaanisha inabidi uanze wewe. Serikali mnafanya mambo kwa “Siri, Udhalimu, Kutowajibika” alafu leo mnahubiri HAKI na MMEUA WALIO ILILIA HAKI? Unatoa wapi UHALALI kutamka UWAZI na UWAJIBIKAJI, wakati hadi leo mmeshindwa tamka MAUAJI, fariji WAFIWA? ZERO EMPATHY! Mnaongelea UHARIBIFU WA MALI. Tume inachuguza NGO badala ya VIFO na MATUMIZI YA RISASI ZA MOTO! Unajisifia umesoma JOURNALISM. Mimi sijasomea, ila mjomba RUDI DARASANI! Journalism Ethics zinaruhusu in Investigative Journalism TO HIDE YOUR SOURCES. Unashangaa CNN kuficha Identity ya NESI? How Ironic for you to say that, na Serikali yako inajaribu kuleta “SHAHIDI WA SIRI” kwenye Kesi ya UHAINI ya TUNDU LISSU. Na hapo Lissu hajaua mtu ka nyie mlioua WATOTO WA KITANZANIA. Kwanini NESI asiogope ku-reveal Identity na nyie mmeua MADAKTARI wakitoka SHIFT YA USIKU? Na sasa hivi Nurses na Morticians wanakamatwa kuhusu video za Mochwari… Waliofanya Uchunguzi waupeleke Tume? Tume imeundwa na SUSPECT na kuipa HADIDU ZA REJEA POTOFU, ndio tuipelekee Uchunguzi, ILI IWEJE? Tume mmeipa Maelekezo ya Kuchunguza “Vijana wanataka Haki gani” na “NGO zilizowalipa” wakati Raia wanataka Majibu na Uwajibikaji wa Nani aliwaua Ndugu zao, na kwanini Miili yao haionekani! Unasema Watanzania wanataka AMANI? Mtanzania gani huyo kakwambia hivyo? Wote wameniambia wanataka: Haki, Maiti Zao, Uwajibikaji, Katiba Mpya, Uchaguzi Mpya, Lissu, Wasiojulikana, Ajira, Tume Huru, Niffer, Mdude, Soka, Polepole, Mwandambo, Haki za Ali Kibao, SamiaMustGo, Free Press, Makanisa ya Gwajima, nk. Girishoni, You’re out of touch! Mitandaoni ni WAJANJA WACHACHE? Hivi hauoni aibu kuzidiwa USHAWISHI na WAJANJA 20 kufanya Serikali kuua Raia Wasio na Hatia zaidi ya 1000, including Wajawazito, Watoto, Mawakili na Madaktari? Eti “tunawaletea MFUKO WA WANAHABARI, Mpate Mikopo kama WASANII.” Yaani huna AIBU unahonga media (BUYING ALLEGIANCE) kwenye Press? Na huo Mfuko wa Wasanii haujaenda kwa Wasanii wenye uhitaji bali CHAWA WENU. You have proved your INCOMPETENCE and being an ACCOMPLICE of the CRIMINAL CABAL of the ILLEGITIMATE GOVERNMENT, way you keep blatantly lying to Us. ICC Bound… SHAME ON YOU GIRISHONI “Akili za kuambiwa changanya na Zako”.. Sisi hatusikilizi mnachotuambia… ZETU ZATUTOSHA The Leader
Webiro Wakazi Wassira #TheLeader66,327 просмотров • 7 месяцев назад

ONENI MAMA YENU (Part One) Yaani SAMIA anaongea kwa kujiamini kabisa kuwa alikuwa anapanga na RUTO jinsi ya kuwapiga na kuwanyamazisha GEN Z sababu wana demand DEMOCRACY, MAENDELEO, AJIRA, UTAWALA BORA na UWAJIBIKAJI. Sababu wao, SERIKALI HARAMU, hawapo tayari kutekeleza hayo, basi wanawageuza Gen Z kuwa MAADUI. Hivi wewe ”Kibibi Yaga” unajua Gen Z ni Watu Wazima? Gen Z wana miaka 15 hadi 30. Ikimaanisha uchaguzi uliopita asilimia 75% ya Gen Z walikuwa Wapiga Kura!! Uchaguzi ujao the youngest Gen Z atakuwa 19 yrs old na kufanya 100% ya Gen Z kuwa Wapiga Kura. They have CIVIC RIGHTS za Kuhoji na Kuwawajibisha. Kwahiyo umeamua kuwa DICTATOR ? Maana KATIBA YA NCHI inasema POWER ya Serikali itatoka kwa Wananchi. Mtanadi sera then tutapiga kura kuchagua tunaowaamini watatusaidia tunachotaka, na MAJORITY WINS. Tukiona hamtekelezi tuna haki ya KUSEMA (Freedom of Expression) na pia tuna haki ya KUGOMA na KUANDAMANA (Right to Demonstrate). Hata Bunge nalo lina haki ya KUGOMA na Kupiga Kura kuondoa Serikali Madarakani kama haiendi na Mwenendo sahihi ambao Wananchi waliowatuma Wabunge, wanataka. Bunge linapiga kura (VOTE OF NO CONFIDENCE) na unaondolewa. Hiyo ndio DEMOKRASIA na sio whatever is in your head. Serikali ambayo hatujaichagua sisi ni HARAMU. Na mnavunja Katiba sio tu kwa kupora Madaraka, bali pia kuendelea kunyanyasa Wananchi. NYIE NI WAHALIFU… Wazungu wanasema MISERY LOVES COMPANY, kwamba umeshajinyea na sasa unataka Ruto akae na wewe ili mnuke wote. Sijui ni uswahili wa “KIFO CHA WENGI SHEREHE”. So unataka kupiga watu kisa wanakukera? tena Watu wazima wanaodai HAKI ZAO? Nasemaje, MTAJUTA KUTUSOMESHA The Leader
Webiro Wakazi Wassira #TheLeader21,230 просмотров • 2 месяцев назад

CRIMINALS CAN NOT INVESTIGATE THEMSELVES Mama Wa Kambo, hiyo Tume umeiunda wewe mwenyewe, ila haina uhalali wa kufanya hivyo. KWANZA SIO RAIS HALALI (Haujachaguliwa na democratic process) Pili, Wewe na Vyombo vya Dola ndio haswa wanapaswa kuchunguzwa, maana ndio the PRIME SUSPECTS wa kilichotokea nchini!! Watu hawajaridhishwa na utendaji wako, na vyombo vyako vya dola vimekuwa vikiteka, vikifira, vikipiga na kuua Raia na pia kuwanyanyasa Wanasiasa wa vyama vya Upinzani. Waliofikwa na Madhila hayo wana ndugu zao, na ndio walioghafirikwa hadi kuandamana. MAANDAMANO SIO UVUNJIFU WA AMANI, Bali again ni nyie nyie mlipoanza kutumia EXCESSIVE FORCE na hatimae hadi kuua Wananchi in intimidation HAPO NDIO MMEVUNJA AMANI!! Mkaanza kufata watu hadi majumbani, na kupiga watu risasi za mgongo (which is against RULES OF ENGAGEMENT let alone usage of Live Ammunitions) HUWEZI KUUNDA TUME ILI UJICHUNGUZE… Hii inaitwa CONFLICT OF INTEREST!! Nakumbuka kwenye Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi, wajumbe walitaka Utoke wao wajadili issue zinazo kuhusu ukagoma (huwezi ku-chair kikao ambacho wewe ni Mgombea). Nakumbuka 2015 Baba yangu Mdogo (Stephen Wasira) alikuwa Kamati Kuu ya CCM, na also alikuwa Mgombea Urais. Ilibidi yeye na Few Other Candidates Watoke kwenye kikao. IT IS LOGICAL. Besides, tumeona kwenye Tume Yako ya Mchongo umemuweka Aliyekuwa Waziri Wa Ulinzi during the Massacre, na ambae ni Kada wa CCM na alikuwa in your campaign. Na kila Mjumbe ni former SUBORDINATE wa Serikali za CCM. Tanzania nzima tumeikataa Tume yako, na hatutaki Tume Za Kimataifa tunazozitaka zijihusishe na Tume yako ya Mchongo kwa Chochote. That is TAMPERING, and it is LEADING… Unataka kuficha UHALIFU WAKO, Unapindisha maneno na Ukweli, na actively mnajaribu kuzika INCRIMINATING EVIDENCE against you and your fellow culprits. MMEANZA KUKAMATA MADAKTARI na BADO MNATEKA VIJANA. Your Evil Scheme will not succeed, na zaidi ni mnazidi tu kujipalia moto na ku-add charges to your already long criminal rap sheet. YOU ARE THE CRIMINAL & THE PRIME SUSPECT, YOU CANT INVESTIGATE YOURSELF, SO TUME YAKO NI BATILI… HATUITAKI NA HATUITAMBUI KAMA AMBAVYO HATUKUTAMBUI WEWE NA SERIKALI YAKO BATILI The Leader
Webiro Wakazi Wassira #TheLeader41,780 просмотров • 7 месяцев назад

Tulianza kama Fans wa each other, tukajakuwa Collaborators, and became Friends later. Tukapishana kauli, then tukaonekana wore haters. Ila mazuri baina yetu yalikuwa mengi zaidi kuliko mabaya, we got cool again and vowed to do big things together again… Haupo nasi tena, ila nimefanikiwa kuikamilisha dream. “Vibe with your tribe…” reach out, and show love! you may never get that chance again. KABILA LETU: Beberu (Declaration) is available on all digital platforms: #Workethic
Webiro Wakazi Wassira #TheLeader111,568 просмотров • 2 лет назад

MWISHO WA USALITI NI KIFO… NI SUALA LA MUDA TU Kwenye Movie ya SARAFINA, kulikuwa na Police mmoja mweusi (SABELA) ambae alikuwa anashirikiana na Makaburu kuwanyanyasa Wanafunzi. Isitoshe ndio alichonga mchongo hadi Mwalimu wa Sarafina, MISS MASEMBUCO anakakamatwa na kuuliwa na Polisi. Walivyokuja kumgundua, wakamuibukia usiku wakazingira nyumba yake kumwambia atoke, alivyogoma wakaiwasha moto! Alivyotaka toroka wakamzingira akala kipigo na mwisho wakamchoma moto. scene ya mwisho baada ya kipigo alivyoinua macho akamuona Sarafina ambae pengine angeweza kuwaambia machizi wasimuue ila alijua kabisa hawezi pata msamaha maana amesababisha Mwalimu wake kauwawa. Usaliti ni kitu kibaya sana, na Wewe unavyokuwa unasaliti unaona uko sawa sababu una enjoy benefits unazopewa na WATESI wa Wananchi, unajiona SAFE! But When THE TABLES TURN, like they always do, inakuwaga too late. Bora upige kimya tu kama wewe ni Benefactor, badala ya kukejeli Wanaharakati, kuwatusi au kusambaza Propaganda ili uwafurahishe ma boss wenu. KUMBUKA, SARAFINA SIO MOVIE, NI TRUE STORY, wakati wa kipindi cha Ubaguzi wa Rangi (APARTHEID) in South Africa, ambapo Wanafunzi 176 waliuwawa kwa silaha za Moto huko SOWETO mwaka 1976. Tanzania nawaona WASALITI na MACHAWA, na WACHUMIA TUMBO (Waandishi uchwara) wakileta shobo and poking their heads out thinking shit is sweet. IT IS NOT UNTIL JUSTICE IS SERVED, The Leader P.S I dont own rights to the clip (Sarafina 1992). It is used for educational purposes only
Webiro Wakazi Wassira #TheLeader33,211 просмотров • 7 месяцев назад
Sensitive content
This media may contain sensitive content.

SIKU ZA MWIZI NI 40: NOW WHAT?! Kwa tukio lililomtokea msaidizi wa Tundu Lissu, kuna mtu yeyote ana doubt juu ya WATEKAJI na WASIOJULIKANA ni kina nani? Kwa namna Polisi wa Mbweni na Mapinga walivyo handle ripoti za tukio walivyozipokea, kuna mtu ana doubt juu ya USHIRIKA WAO kwenye utekaji na kupotosha ukweli? Tendo la Watekaji kukimbilia eneo ya Usalama wa Taifa, kisha kwa kujiamini na kuanza kupiga risasi upande wa Wananchi, kuna mtu yeyote ana doubt USHIRIKI wa USALAMA? Vyombo vya Ulinzi na Usalama kwa kawaida huwa vinaundwa na watu wenye AKILI, na wanaotumia Akili na sio MABAVU; Ndio sababu vinaitwa INTELLIGENCE AGENCIES. Ila the minute you use FORCE, unaanza kufanya kazi isiyo na efficiency, na hatimae wanaanza kutoa maboko hadi wanajianika hadharani. Na Wananchi toka mmeanza kuwapiga risasi, hamkuwaza kuwa watazoea na wataanza kuwa HAWAOGOPI, na watawafukuza hadi mwisho muendapo… Tunaomba JAJI CHANDE akaongeze hii Story ya Djumbe, kuwa alitekwa sababu ya Mapenzi na Ushirikina na Akapigwa nusura kufa na kufungwa pingu. Kaongeze hii kwenye hiyo ripoti ya Mama Wa Kambo! CCM na SERIKALI YENU HARAMU nchi imewashinda, please ondokeni maana mnaanza kuhatarisha amani ya nchi yetu. TUMEWACHOKA, HATUWATAKI, HATUWATAMBUI Nina laani vikali Utekaji wa Djunbe, na naomba Watanzania wote tuwe on high alert ready to fight back kuanzia sasa, WATATUMALIZA tusipolindana. Pole kwa Djumbe, familia na marafiki walioathirika wakati wa tukio. Ila Pongezi za dhati kwa Bodaboda na Wananchi wengine waliosaidia kupambana na Watekaji hao. The Leader
Webiro Wakazi Wassira #TheLeader10,489 просмотров • 1 месяц назад

MAMA WA KAMBO ACHA UONGO! Wewe binafsi umehuzunishwa na nini? Watu wamekufa 2 weeks ago, na wameuliwa na Askari ambao unajitapa kuwa wewe ndio Amri Jeshi Mkuu, na isitoshe ukaja na kuilaghai Dunia kuwa walikuwa Raia wa Kigeni, na on top of it ukaweka vitisho vya kutumia Nguvu zaidi kwa anaovunja amani… IWEJE LEO GHAFLA useme umehuzunishwa?! A genuine being hawazi address This Massacre kirahisi hivyo. USITUFANYE WATOTO Sasa unawapa pole ya nini hao "Wavunja Amani"? Unawapa ugua pole ya nini? Unataka kuchunguza nini wakati Vyombo vya usalama vina move by "your orders" ? UNATAKA KUJICHUNGUZA MWENYEWE ?! How credible are your words? Mind you UCHAFUZI wenu kila mtu duniani ameuona (Kujipa 98% winning ya 30 million votes, in a day without participation ya Key Parties/Candidates, na with Maandamano on top of it, na Ballots zilizoharibika kwa vituo kuvamiwa na vurugu) HIVI MNATUONA SISI NI WAJINGA SANA ?! It is obvious the pressure is mounting in on you, and you are trying to save face. IT IS TOO LATE… MARIDHIANO PEKEE NI KWA WEWE NA SERIKALI ILLEGITIMATE KUACHIA NGAZI NA WAUAJI WACHUKULIWE HATUA. Na hatutaki Uchaguzi wowote Mpaka Tupate KATIBA MPYA Hatutaki Uchunguzi kutoka kwenu; you are the culprits! You are Guilty of Mass Killings, Stealing the Elections, and Illegitimately forming a Sham Government! HATUWATAKI NA HATUWATAMBUI The Leader
Webiro Wakazi Wassira #TheLeader34,234 просмотров • 7 месяцев назад

WE CHALAMILA DAR HAKUNA MZEE NA NCHI HAINA RAIS! Oneni huyu Pampula anavyoleta habari za kiduanzi. SIKILIZA MJOMBA… Dar Hakuna MZEE, Wazee wa Dar ni GEN Z! Uzee mwisho Chalinze, so kama anataka aende MSOGA huko ndio akaongee na Wazee. Pili, Sisi wengine wote HATUMTAMBUI wala HATUMTAKI huyo RAIS HARAMU, MWIZI WA UCHAGUZI, asiye na UTU na MUUAJI WA WATOTO WA TANGANYIKA. SAMIA na GENGE LAKE, ni MAGAIDI, WAHAINI, WAUAJI… Tuachie Nchi yetu, nenda katafute nyingine ya kuichezea sio yetu. Huyu Mlevi anatwambia “Nchi inarejea kwenye Amani” huku anamnadi aliyeivunja Amani ya nchi kwa kuua WATOTO?! Kamtuma Yule Mlughalugha MADELU asambaze Propaganda, ndio anataka jitokeza kuongea. TUTA DEAL NA NYINYI VYEMA TU… WANYALUKOLO HUU MWEZI MMETUANGUSHA SANA. Smh We will not stop until justice is served!
Webiro Wakazi Wassira #TheLeader32,110 просмотров • 7 месяцев назад

I wouldn’t recommend any serious artist kumjibu… Uwezo unapimwa kwa utakachofanya na artist in the same record, na for lack of better words, “KHALIGRAPH umekuwa unakimbia ku-rap na TZ LYRICAL TITANS” We celebrate you as a successful EA eMCee, ila haumtishi mtu huku. Facts!!
Webiro Wakazi Wassira #TheLeader103,206 просмотров • 2 лет назад

ROSA REE: Criticize, but dont get entitled! Stop the ENTITLEMENT please! Umetoa wimbo mmoja unahisi unastahili kuwa “Best of the Year” over Nash MC na Nikki Mbishi ambao wana Albums ?! Tuzo zina flaws yeah, and I think the nomination you deseved was that of “Best Rap Song” ila lets not be too entitled. If you got a nomination be grateful. Unge make sense kama ungeamza kwa kusema, “SIDHANI KAMA NINA STAHIKI CATEGORY NILIYOWEKWA, ILA YA WIMBO BORA NDIO NINASTAHILI” hapo ningeelewa ila sio ufurahie category na ulalamike zingine… come on Your diss song (Mama Omollo) was Dope, but so was Freshlikeuhhh’s (Dear Brian)… ila Darassa has a bigger song “Nobody” ft Bien na haujawa nominated. Au Darassa sio Rapper? 🤷🏾♂️ “Nobody” imetoka 2 months before you, na bado hadi sasa inawika(commercially ime hit zaidi, na viewership imekuzidi 4x) ! KUMBUKA!! Wanaangalia miezi 12 ya mwaka sio tu wimbo ulioutoa mwisho wa mwaka ukawa na hype ya mwezi! Remember that Let’s call out mapungufu ya Tuzo zetu, ila not from an Entitlement standpoint. Please Na pia acheni mambo ya kushukuru serikali, sijui nini… Let’s talk about Art. Tuzo ni za Muziki, na kama serikali inahusika basi ni imetekeleza wajibu. Sasa hapo unaishukuru kwa nini ikiwa unalalamika still? Respectfully, The Leader
Webiro Wakazi Wassira #TheLeader56,908 просмотров • 1 год назад

Nimesha kesha, usiku kama Popo, na Wapopo Sio Issue, Askari halali, Jenerali mpaka Corporal Tafuta fedha halali, “gettin’ bread” tena Boflo All you MOFOs, steady hatin’, hopin’ for my DAWN-fall I mean “down”, kwenye game, I’m in now Tuliyopitia, we persevered, Thank God, Amina Waliotangulia, “Innah lillahi wa innah Ilayhi rajiun” Hii Safari tunafatana kama July na June…. ©️ Wakazi Lady Jaydee ft. Rapcha, Frida Amani & Wakazi - Po Po Remix:
Webiro Wakazi Wassira #TheLeader24,406 просмотров • 1 год назад

Yote yalishasemwa… ROMA MKATOLIKI #TZHipHop
Webiro Wakazi Wassira #TheLeader13,381 просмотров • 6 месяцев назад

HII NDIO SABABU MICHEZO HAIKUI BONGO: SIASA NYINGI Huyo “Kiziro” MAKONDA anaenda kuongea na TAIFA STARS ili iweje? Kwanini tunaendekeza WANASIASA sana kwenye vitu hivi? Kwanza ni WAZIRI HARAMU, maana ametokana na SERIKALI HARAMU ya SAMIA ambae AMEIBA UCHAGUZI na kuidhinisha Maelfu ya Watoto wa Kitanganyika kuuwawa kwa SILAHA ZA MOTO ili yeye abaki Madarakani. Mataifa mengine, Wanaalikwa WACHEZAJI WA ZAMANI (Accomplished), Watu Mashuhuri Kihistoria waliowahi kabiliana na Ukinzani wakashinda, Wanajeshi wenye “Medals Of Honor”, Cancer Survivors, Makocha legendary, etc ili Wachezaji wawe INSPIRED. Sisi anaenda kuongea Mwanasiasa anayetafuta Legitimacy & Relevance, na inspiration yake ni “Mkishinda tunawapa Tsh MILLION 300” Clip hiyo SAMUEL ETO’O anaongea na kikosi cha Cameroon, na kuwaambia wacheze kwaajili ya Bendera ya Taifa na Pride ya Nchi, sisi tunawaambia vijana wetu tutawapa HELA!! Yaaani NJAA zetu (ambazo wao wao ndio wametupa) wanazitumia kama SILAHA kila wakitaka kutuchota akili na kutupumbaza. Sasa ukifanya Timu yako iwe inanunulika kirahisi hivyo, no loyalty, no integrity… inamaana akitokea mtu mwenye DAU KUBWA wanauza Mechi. 🤷🏾♂️ Million 300? ni sawa na Dola $125,000. Hiyo ilikuwa ni cheque ya One Week ya HASHEEM THABEET wakati anacheza NBA (I was there I saw it). Sasa team nzima ndio igawane hiyo… Alafu Waziri Mzima anasema kama vile ametaja bonge la hela. Na anapiga Siasa kabisa “tunaweza wawekea kwenye account kabisa, tubaki sisi kuwadai ushindi”. Tuna Ex-Players kibao ambao wanaweza kuwa good MENTORS wa Madogo, ila unakuta msafara huko wameenda Viongozi na Wanasiasa, na maswahiba zao kama sio Michepuko yao. BORESHENI VIWANGO VYA MCHEZO, MIUNDO MBINU, FACILITIES, TREATMENT na WALIMU, ili Soccer ikue kweli. Pia fundisheni madogo UZALENDO na THAMANI YA KUCHEZEA TAIFA, badala ya kuwa ENTICE na vihela mbuzi. Tatizo nyie wenyewe Uzalendo hamna ndio maana mnabagaza Katiba, Mnaua Watoto wa Wenzenu na kuwaweka Jela…. na ndio maana mnahangaika kuji sanitize na HELA ZA KUHONGA na SIASA ZA KITOTO. Hamna legit plans za long term, ni tia maji tia maji tu… hovyo kabisa! Btw, huyo Naibu Waziri, namuita Kiziro sababu alipiga Div 0 NECTA! Na pia Mipango yake daily huwaga inafeli… so ni dhahiri akili ndogo sana anatumiaga 🤓 The Leader
Webiro Wakazi Wassira #TheLeader11,681 просмотров • 6 месяцев назад

Soundtrack ya hii post 👇🏾 Motra The Future ft Medusa - WAKRISLAM: Motra ni miongoni wa Wasanii Baadhi waliosimama upande wa Wananchi, wa Ukweli na Haki. Huu wimbo ni katika sehemu ya kukemea na kuwapinga Wachungaji na Mashehe UBWABWA #SupportYourOwn
Webiro Wakazi Wassira #TheLeader12,623 просмотров • 7 месяцев назад