Video yükleniyor...

Video Yüklenemedi

Ana Sayfaya Dön

62,356 görüntüleme • 17 gün önce •via X (Twitter)

0 Yorum

Yorum bulunmuyor

Orijinal gönderinin yorumları burada görünecek

Benzer Videolar

Tofauti na mitazamo ya baadhi ya wanachama wa CCM na wachambuzi wa siasa waliokuwa wakidai kuwa CHADEMA imepoteza mvuto na inaelekea ukingoni mwa siasa za Tanzania, ziara ya viongozi wake wakuu katika mikoa ya Mbeya na Njombe imeonesha picha tofauti baada ya maelfu ya wananchi kujitokeza katika mikutano ya hadhara iliyofanyika katika maeneo mbalimbali ya mikoa hiyo. Ziara hiyo inayoongozwa na Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara John Heche pamoja na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Zanzibar, imevutia umati mkubwa wa wananchi waliofurika katika viwanja vya mikutano tangu saa kadhaa kabla ya viongozi hao kuwasili. Katika baadhi ya maeneo, wananchi walionekana wakisongamana kandokando ya barabara na viwanja vya mikutano ili kupata nafasi ya kusikiliza ujumbe wa viongozi hao. Mbali na mahudhurio makubwa, jambo lililoibua mjadala ni mwitikio wa wananchi katika uchangishaji wa fedha za chama kupitia kampeni ya “Tone Tone”, mamia ya wananchi wakionekana kujitokeza kwa hiari kutoa michango yao, huku wengine wakisukumana kuelekea jukwaani ili kukabidhi michango yao mbele ya viongozi wa chama hicho. Baadhi ya wananchi waliozungumza baada ya mikutano hiyo walisema wamehamasishwa na ujumbe wa viongozi wa CHADEMA kuhusu demokrasia, uwajibikaji na mustakabali wa taifa, hali iliyowafanya waone umuhimu wa kuchangia shughuli za chama. Walisema michango yao, licha ya kuwa midogo kwa baadhi yao, ni ishara ya kuunga mkono harakati wanazoamini kuwa zina manufaa kwa jamii. Wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanasema mwitikio huo katika mikutano ya Mbeya na Njombe unaonesha kuwa ushindani wa kisiasa nchini unaendelea kuwa hai, huku vyama vya upinzani vikionesha uwezo wa kuhamasisha wananchi na kukusanya rasilimali kupitia michango ya wanachama na wafuasi wao.

Royal Media

14,694 görüntüleme • 5 gün önce