Sensitive content

This media may contain sensitive content.

Loading video...

Video Failed to Load

Go Home

BeriGalaxy / Jerbear

162,646 views • 1 year ago •via X (Twitter)

0 Comments

No comments available

Comments from the original post will appear here

Related Videos

"Kuondolewa kwangu kama mnavyojua zilianza shida ndogo ndogo zile za Trilioni moja na nusu, halafu Spika Ndugai akaleta mazungumzo yale mpaka mwisho nikahisi tu mimi mwenyewe na unajua Tanzania hii ni Nchi ndogo sana, unapewa taarifa mapema kwahiyo kuna mtu akaniambia sasa hivi wameanza mchakato aa kumtafuta CAG mwingine. "Ukisoma katiba inasema kustaafu ni miaka 60 au umri wowote utakaoelekezwa na sheria. Sheria ya ukaguzi inasema miaka 65 kwahiyo ukiisoma katiba moja kwa moja unaona kuwa haiwezekani kustaafu. Na hili halikuwa jambo la hisia bali ni jambo la tafsiri ya katiba. Nikasema kwamba hapa kuna tatizo." "Nakumbuka nilikuwa Mwanza kwenye shughuli, akanipigia yuleyule Bwana aliyeniambia kuwa wameanza kutafuta CAG mpya, akaniambia unaenda kuondolewa kesho asubuhi na nina taarifa za ukweli kabisa kutoka kwenye Mamlaka. Nikashukuru tu na kusema hatukuzaliwa kukaa kwenye nafasi hizi, ikitokea mwenyenzi Mungu amejalia tuondoke tutaondoka tu. Imefika asubuhi Jumapili, kijana mmoja wa idara akanipigia kuniambia nimeona tangazo la Katibu Kiongozi kuwa saa moja baadae utaondolewa." "Nilikuwa na gari la serikali Mwanza, palepale kabla taarifa ya mimi kuondolewa haijatangazwa nikwambia dereva rudisha gari Dodoma mimi nitarudi Dar Es Salaam mwenyewe kwa ndege. Baada ya saa moja nikamsikia Kijazi kweli anatangaza." .... Jumatatu nikaenda Ofisini nikapaki gari yangu binafsi chini (IST nyekundu) nikaingia mapokezi, Kijana wa mapokezi ananiambia kuna watu juu Ofisini kwako nahisi hutoruhusiwa kuingia, nikwambia no, kwasababu leo ni tarehe nne na niliajiriwa tarehe tano basi bado mimi ni CAG technical, nikapanda juu ghorofa ya tatu, natokea tu pale nakutana na vijana wawili wanasema wameagizwa kukaa pale kulinda ofisi hivyo ni vigumu sana mimi kuingia, nilipowauliza maagizo yametoka wapi wakasema yametoka Ikulu. .... Kwakweli nilitoka pale nimekasirika kidogo kuhusu utaratibu wa kunifukuza Ofisini wakati sijamaliza muda wangu na sijapewa barua rasmi." Amesema Prof. Mussa Juma Assad, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) mstaafu wakati akizungumza na Runinga mtandao ya M/s Podcast.

Royal Media

37,074 views • 8 days ago