Загрузка видео...
Не удалось загрузить видео
millardayo Sababu ya kufungiwa
36,582 просмотров • 1 год назад •via X (Twitter)
Комментарии: 11

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limesema limejiridhisha kuwa Seif Kassim Kisauji maarufu Babu wa TikTok ametenda kosa la kimaadili wakati akitekeleza kazi zake za sanaa na limefikia maamuzi kumfungia kutokujishughulisha kufanya kazi za sanaa ndani na nje ya Tanzania kwa kipindi cha miezi sita kuanzia leo July 22,2024 na kumtoza faini ya Tsh. milioni 3 ambayo anatakiwa kuilipa ndani ya siku 7 kuanzia leo. Baraza limesema limefikia uamuzi huo baada ya kumuita Kisauji kuhusiana na ukiukwaji wa maadili akiwa kama Msanii aliyesajiliwa na Baraza la Sanaa la Taifa kwa usajili Na. BST-9684-2023-2154 ambapo ukiukwani huo wa maadili ni kinyume na Kanuni ya 25 (6) ya Kanuni za Baraza la Sanaa la Taifa za mwaka 2018 na Mwongozo wa Uzingatiaji wa Maadili katika Kazi za Sanaa wa Mwaka 2023. “Baraza la Sanaa la Taifa kupitia Sheria Na. 23 ya Mwaka 1984 na Maboresho yake ya Mwaka 2019 ina mamlaka ya kusimamia maadili ya msingi kwenye Sekta ya Sanaa kwa Kanuni ya 25(1)-(8) ya Kanuni za Baraza la Sanaa la Taifa za Mwaka 2018” “Baraza limekwishatoa na kuzindua mwongozo wa maadili katika kazi za sanaa ambao unapatikana katika tovuti yetu hivyo ni jukumu la kila Msanii na Mdau wa Sanaa na jamii kuzingatia maadili katika kazi za sanaa” #MillardAyoUPDATES

@millardayo Huyu Mzee anafamilia kweli ? Mke, watoto, wajukuu? Tuianzie hapa .... Maana hii pia inaweza kuwa afya ya akili si bure, Mzee wa haya makamo haya kufanya ujinga huu na wajukuu ni hatari Sana.

@millardayo Hawa mabinti walikamatwa lakin?

@millardayo @ZephilineEze hiyo hapo ibamnyonga😂😂😂

@millardayo Nyieee🤣🤣

@millardayo Mzee Kapagawa na hela ya tick tock na hela yenyewe ikamtia kitanzi🤣🤣🤣🤣Use your money wisely Babu

@millardayo vitoto vya 2000 vina balaa

@millardayo Daaah hiki si kitoto kabisa

@millardayo Mzee hana familia😳

@millardayo Wamfungie tu hana adabu

@millardayo huyu mzee nilijuaga atakuja kukiingia tu cha kumdhalilisha
