Video wird geladen...

Video konnte nicht geladen werden

Zur Startseite

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kilolo.

84,445 Aufrufe • vor 4 Tagen •via X (Twitter)

0 Kommentare

Keine Kommentare verfügbar

Kommentare vom Original-Post werden hier angezeigt

Ähnliche Videos

Taasisi ya Flaviana Matata ikiambatana na Shirika la Uratibu na Maendeleo la Uturuki (TİKA), wamezindua na kukabidhi mradi wa matundu 12 ya vyoo, sehemu ya kunawia mikono, chumba kwa ajili ya Wanafunzi wenye mahitaji maalumu, chumba maalumu kwaajili ya Wasichana kujisitiri wakiwa kwenye siku zao za hedhi, pamoja na sehemu ya kuchomea taka hususani taulo za kike zilizokwisha kutumika uliotekelezwa na Taasisi ya Flaviana Matata kwa udhamini wa Ubalozi wa Uturuki katika Shule ya Sekondari Mbezi Juu Jijini Dar es salaam. Akiongea leo May 15,2025 Mkurugenzi wa Flaviana Matata Foundation, Mwanamitindo Flaviana Matata (Flaviana Matata) amesema hatua hiyo ni katika kuendelea kuunga mkono jitihada za Serikali, hususani kwenye nyanja ya elimu na afya na kukuza juhudi za kutatua changamoto zinazowakabili Wattoo wa kike katika kufikia ndoto zao, kwa kuhakikisha wanapata mazingira salama, rafiki na jumuishi ya kujifunzia. Amesema mradi huu utanufaisha jumla ya Wanafunzi takribani 1,304 kila mwaka katika Shule ya Sekondari Mbezi Juu, pia miundombinu hii itatatua changamoto ya muda mrefu ya uhaba wa vyoo, kichomea taka na upatikanaji wa maji Shuleni hapo. Hafla ya Uzinduzi huu imehudhuriwa na Mgeni Rasmi, Balozi wa Uturuki, Bekir Gezer, Mkurugenzi wa Shirika la Uratibu na Maendeleo la Uturuki (TİKA), Bi Filiz Sahinci, Mkurugenzi wa Taasisi ya Flaviana Matata, Flaviana Matata akiambatana na Viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kinondoni, Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Kinondoni pamoja na Walimu, Wanafunzi na Wadau mbalimbali ambao wanatekeleza miradi ya maji na usimamizi wa usafi ya WASH nchini Tanzania. #MillardAyoUPDATES

millardayo

94,152 Aufrufe • vor 1 Jahr

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Adam Malima, ametoa wito kwa madiwani kuhakikisha wanawahamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025, huku akisisitiza umuhimu wa kudumisha amani na kutoruhusu vitisho vya aina yoyote kutoka kwa watu wanaopandikiza hofu. Akizungumza katika kikao maalum cha kupitia na kutathmini hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) katika Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga, Malima amesema kuwa ni wajibu wa kila raia kutimiza haki yake ya kikatiba kwa kupiga kura kwa utulivu na amani. Katika hatua nyingine, Malima amewataka madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi pamoja na uongozi wa halmashauri hiyo kuhamasisha wananchi kulima mazao ya kimkakati kama Kakao, Karafuu na Parachichi,ambapo hatua hiyo inalenga kuchochea mapinduzi ya kilimo na kukuza uchumi wa jamii husika kupitia sekta ya kilimo. Kwa upande wake, Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Morogoro, Nuru Ngereja, amewapongeza madiwani wa halmashauri hizo kwa kushirikiana vyema na ofisi ya CAG katika kupitia hoja na kupanga mikakati ya maboresho. Nao baadhi ya madiwani wameahidi kwenda kutekeleza kwa vitendo maelekezo yote waliyopewa ili kuimarisha uwajibikaji na maendeleo katika maeneo yao. Aidha, katika vikao hivyo vya tathmini ya hoja za CAG, Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga ina hoja 15, huku Halmashauri ya Malinyi nayo ikiwa na hoja 15. Malima amesisitiza kuwa kutatuliwa kwa hoja hizo ni nafasi ya kuboresha utendaji na kuimarisha usimamizi wa rasilimali za umma.

Jambo TV

11,681 Aufrufe • vor 1 Jahr