Sensitive content

This media may contain sensitive content.

Video wird geladen...

Video konnte nicht geladen werden

Zur Startseite

44,278 Aufrufe • vor 1 Jahr •via X (Twitter)

0 Kommentare

Keine Kommentare verfügbar

Kommentare vom Original-Post werden hier angezeigt

Ähnliche Videos

Mwandishi wa habari Alloyce Nyanda amesema Tanzania haiwezi kuongozwa kwa misingi ya “zamu za dini,” akisisitiza kuwa viongozi wanapaswa kuchaguliwa kwa kuzingatia uwezo, uadilifu, uchapakazi, maono na uwezo wao wa kulitumikia Taifa. Nyanda amesema hayo katika mtazamo wake aliouchapisha kupitia mitandao ya kijamii, akisema hakuna msingi wa kuamua mgombea wa upinzani awe wa dini fulani kwa sababu tu Rais anayetawala anatoka dini nyingine. Amesema hoja ya kwamba iwapo chama tawala kina Rais Mkristo basi mgombea wa upinzani lazima awe Mwislamu, au kinyume chake, inaweza kuwa na madhara kwa Taifa endapo itatumika kama msingi wa kuchagua viongozi. “Kiongozi anapaswa kuchaguliwa kwa uwezo wake, uadilifu wake, uchapa kazi wake, maono yake na uwezo wake wa kulitumikia Taifa, si kwa sababu ya dini yake,” amesema Nyanda. Amesema Tanzania inaweza kujikuta katika mazingira ambayo mtu asiye na sifa za uongozi anapewa nafasi kwa sababu tu jamii inaamini kuwa ni “zamu” ya dini yake kuongoza. Nyanda amehoji iwapo Watanzania wataendelea kumuunga mkono kiongozi anayehusishwa na vitendo vya ubadhirifu au ufisadi kwa sababu tu anaaminika kuwa ni zamu ya dini yake. “Je, ikiwa huyo anayesemwa kuwa ni ‘zamu yake’ ni mwizi au fisadi wa mali za umma, tutaendelea naye kwa sababu tu ni zamu ya dini yake?” amehoji. Amesema Taifa linapaswa kujengwa kwa misingi ya uwezo, uadilifu, uwajibikaji na maslahi mapana ya Watanzania badala ya kuangalia dini ya mtu wakati wa kufanya maamuzi ya kisiasa. Kwa mujibu wa Nyanda, mjadala wa uongozi wa Taifa unapaswa kuangalia sifa na uwezo wa mtu wa kuwatumikia wananchi, huku akionya dhidi ya viongozi wanaoweza kutumia hoja ya dini kama msingi wa kupata uungwaji mkono. “Taifa haliwezi kuongozwa kwa zamu za dini; linapaswa kuongozwa kwa misingi ya uwezo, uadilifu, uwajibikaji na maslahi ya Watanzania,” amesema. Amesema Watanzania wanapaswa kuwa makini na viongozi wanaoanzisha au kuendeleza mijadala ya kugawanya jamii kwa misingi ya dini, akisisitiza kuwa kiongozi anayefanya hivyo anapaswa kukataliwa. “Ukianza kuona mjadala wa namna hiyo huyo kiongozi mkataeni haraka, ni muhuni,” amesema Nyanda.

Royal Media

46,087 Aufrufe • vor 14 Tagen

Ada yg mau jadi gym partner?
0:27

Sensitive content

Ada yg mau jadi gym partner?

Yuanita

113,267 Aufrufe • vor 4 Monaten