正在加载视频...

视频加载失败

Walimu tuna pesa, msituone hivyo 😂

112,784 次观看 • 1 年前 •via X (Twitter)

11 条评论

Baba Faith. 的头像
Baba Faith.1 年前

Hata kama Kuna mwalimu alinichapa miaka hiyo Leo nikimuona naona fahari sana sababu alinitoa ujinga angalau Leo naweza kusoma Hata Alama za Barabarani hata kama Sina Hela namheshimu sana mtu anaitwa mwalimu pa1 na utundu wangu uliopitiliza lkn alinivumilia.

Solar Heavy 的头像
Solar Heavy1 年前

you like new space laced bass music?

mimi 的头像
mimi1 年前

wanadhalilika but they are doing great as parents as well. kwa ground huwezi elewa kama hawa parents and teachers namna wako na hali ngumu ndiyo umepita kwao uwe tajiri na hadhi kubwa.

Masubi 的头像
Masubi1 年前

@TweetHelperBot download this video

krogstad 的头像
krogstad1 年前

Tf 😭😐😂🤚

Lekey 的头像
Lekey1 年前

🤣🤣🤣

Jjosh Ogonji 的头像
Jjosh Ogonji1 年前

That part uliingia madawa🤣

kags 的头像
kags1 年前

@kah1ga mchuna bana😂

MR.SILAYO👑👑👑 的头像
MR.SILAYO👑👑👑1 年前

Na uliingia madawa eh ila waalimu wa hesabu duh😄😄

kev the red 的头像
kev the red1 年前

Distasteful content

captain 的头像
captain1 年前

😅😅😅

相关视频

VIDEO: Katika hali ya kushangaza, walimu wa Shule ya Msingi Nkweshoo iliyopo Kijiji cha Mkuu Ndoo, Kata ya Machame Mashariki, wilayani Hai, mkoani Kilimanjaro, wanadaiwa kuomba uhamisho kwa madai ya ubaguzi kutoka kwa baadhi ya wazazi wa wanafunzi wanaosoma shuleni hapo. Shule hiyo yenye walimu saba inadaiwa kuwa na mgogoro kati ya baadhi ya wazazi na walimu, ambapo inasemekana wazazi wanataka shule hiyo ifundishwe na walimu wazawa, hali iliyowafanya walimu wote kuomba uhamisho. Hata hivyo, Mkuu wa Shule hiyo, Mwalimu Method Haule, amekanusha madai hayo akisema kuwa taarifa hizo si za kweli na zimeleta taharuki isiyo na msingi. Ameeleza kuwa hajawahi kutoa takwimu wala taarifa zozote zinazoashiria hali hiyo shuleni kwake. Kwa mujibu wa taarifa, hali hiyo ilifikia hatua ya kujadiliwa katika kikao cha Halmashauri ya Kijiji kilichofanyika Ijumaa iliyopita, ambapo wazazi na viongozi wa kijiji walikutana kutafuta ufumbuzi wa madai kwamba mmoja wa walimu alifanyiwa vitendo vya kishirikina kwa kurushiwa mawe kwenye paa la nyumba yake. Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu ya kijiji hicho, Elimwaria Mbora, amenukuliwa akisema kuwa ni kweli baadhi ya walimu waliomba uhamisho kutokana na changamoto zilizojitokeza, ingawa hakufafanua zaidi kuhusu hali hiyo. Diwani wa Kata ya Machame Mashariki, James Mushi, pamoja na madiwani wa viti maalum wa eneo hilo, wameelezea kusikitishwa na taarifa hizo, wakisisitiza kuwa wakazi wa eneo hilo wanaishi kwa amani na walimu wa shule hiyo, na hakuna mgogoro wowote wa wazi baina yao. Shule hiyo yenye jumla ya wanafunzi 168 ina walimu saba, ambapo watano ni wa ajira rasmi huku wawili wakiwa ni wa mafunzo kwa vitendo. Mpaka sasa, mamlaka husika bado hazijatoa tamko rasmi kuhusu suala hilo, lakini inatarajiwa kuwa litapatiwa ufumbuzi wa haraka ili kuepusha athari kwa maendeleo ya elimu katika eneo hilo.

Jambo TV

27,110 次观看 • 1 年前