Sensitive content

This media may contain sensitive content.

Video yükleniyor...

Video Yüklenemedi

Ana Sayfaya Dön

132,575 görüntüleme • 3 yıl önce •via X (Twitter)

0 Yorum

Yorum bulunmuyor

Orijinal gönderinin yorumları burada görünecek

Benzer Videolar

Huyu ni Simai Mohamed Said Mbuge wa Jimbo la Tunguun (Zanzibar) Wasilisho la mbunge huyu leo hii akichangia bajeti ya wizara ya fedha, limebainisha dhahiri ndani ya serikali kuna msigano mkubwa. Mbunge huyu alitoka kabisa nje ya mada kuchangia hoja iliyokuwepo mezani na kuanza kumshambulia mtu anayedai yupo ndani ya serikali kwa kumuita Yuda Kwa mujibu wa video hii, Mbuge huyu anamtaja Yuda kwa sifa zifuatazo 1. Anatumia vibaya nafasi ya kuaminika na rais kumsaliti 2. Mtu huyo amefitini watu ambao walikuwa wanakaa siti za mbele bungeni (mawaziri) na sasa wako backbench. Amefitini sana wafanyabiashara na kupotezea wengi ndoto zao za kisiasa. 3. Mtu huyo amekuwa akilitumia kanisa kuifitini serikali Hadi hapa nilikuwa nimetatizika sana kumjua mtu wenye wasifu hapo juu. Lakini mbunge huyu akanirahisishia kazi alipoongeza kuwa 4. Yuda anajidai alikuwa anapendwa na hayati Magufuli wakati enzi za utawala wake alimtupa mbali huko nje ya nchi. Hili halikuwa tena fumbo kwangu. Ni hivi karibuni, katika msiba wa mama mzazi wa hayati rais Magufuli, John Nchimbi, Makamu wa rais, amenukuliwa akielezea jinsi alivyokuwa karibu na hayati Magufuli wakiitana watani. Jinsi alivyokuwa akichukua pipi za Magufuli kwa kuwa hakuwa akila pipi, jinsi alivyotaka kumteua ubunge kupitia nafasi 10 anazopewa rais, na hadi jinsi alivyomteua balozi japo alishamwambia nia yake ya kutaka kupumzika. Nchimbi katika kutaka kuthibitisha hili, akaomba wasaidizi wake wamletee simu yenye ujumbe aliotumiwa na Magufuli ambao ameutunza mpaka leo na aliuonyesha kwa familia yake yote. Kwa hiyo, mbunge huyu Mzanzibari ameshaanza kutupa code kuwa kuna kutoaminiana ndani ya viongozi wa juu wa serikali. Nachelea kusema mbunge huyu hakuingea haya kwa bahati mbaya bali imetokana na vikao vilivyofanyika sehemu na kuaminishana haya aliyoyaongea leo, na ametumwa kuyawasilisha. Ujumbe mwingine unatumwa hapa ni vita dhidi ya kanisa ambalo halijatajwa. Kama alimaanisha kanisa la Nchimbi, basi kuna vita visivyo vya wazi kati ya watu fulani ndani ya serikali na Kanisa Katoliki. End of evening rant

Fortunatus Buyobe

46,623 görüntüleme • 1 ay önce