ๆญฃๅœจๅŠ ่ฝฝ่ง†้ข‘...

่ง†้ข‘ๅŠ ่ฝฝๅคฑ่ดฅ

๐‡๐ฎ๐ฎ ๐ง๐ข ๐ฆ๐ฎ๐๐š ๐ฐ๐š ๐ค๐ฎ๐ซ๐ฎ๐๐ข๐ฌ๐ก๐š ๐ฎ๐ฌ๐ก๐ข๐ง๐๐ข ๐ง๐ฒ๐ฎ๐ฆ๐›๐š๐ง๐ข. Shinda zawadi mbalimbali kama simu, pesa taslimu, tablet, fridge kali, safari za kwenda nje ya nchi na zawadi kubwa ya ndinga; ๐๐Œ๐– ๐—1, ๐Œ๐ฉ๐ฒ๐š๐š๐š๐š๐š๐š๐š kwa ajili ya mishe zako.

279,443 ๆฌก่ง‚็œ‹ โ€ข 2 ๅนดๅ‰ โ€ขvia X (Twitter)

6 ๆก่ฏ„่ฎบ

NBCTanzania ็š„ๅคดๅƒ
NBCTanzania2 ๅนดๅ‰

Unachotakiwa kufanya ni; Fungua akaunti yako sahihi, weka akiba, uwe kwenye droo ya kushinda ndinga kali na mazawadi kibao. Droo zitachezwa kila mwezi na droo kubwa ya kushinda ๐๐Œ๐– ๐—1 itafanyika kila baada ya miezi 3. Kama unayo akaunti ya NBC tayari fanya kuweka maokoto kadri uwezavyo ili ushinde mechi zako. Tembelea tawi la NBC lililopo karibu yako Au piga 0800 711 177 (BURE). #ShindaMechiZako

Baritone Tz ็š„ๅคดๅƒ
Baritone Tz2 ๅนดๅ‰

Visual ๐Ÿ™Œ

Dave Eas+ ็š„ๅคดๅƒ
Dave Eas+2 ๅนดๅ‰

Mbona nikitaka kutuma pesa kutoka kwenye sim kwenda kwenye account yangu ya NBC naambiwa account number sio sahihi??? Naomba majibu tafadhari

PureArch ็š„ๅคดๅƒ
PureArch2 ๅนดๅ‰

Njoo tukuchoree Ramani

Rasiael Nicholaus ็š„ๅคดๅƒ
Rasiael Nicholaus2 ๅนดๅ‰

NBC juu sanaaa tunawakubali mmeiwezesha Burudani mmenogesha Sana

arrafa alfani ็š„ๅคดๅƒ
arrafa alfani2 ๅนดๅ‰

Nicheki Kwa Whatsap 0717778770

็›ธๅ…ณ่ง†้ข‘

Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya amesema Serikali inapaswa kuongeza nidhamu ya matumizi ya fedha za umma kwa kupunguza matumizi ya magari yanayotumia mafuta kwa kiwango kikubwa, ikiwemo yenye Injini kubwa kama V8, ili fedha zaidi zielekezwe kwenye miradi ya maendeleo. Akichangia Bajeti ya Serikali katika Bunge la Kumi na Tatu, Mkutano wa Tatu, Kikao cha Hamsini leo Juni 16, 2026, Bulaya amesema bajeti inayotarajiwa kupitishwa ina kiwango kikubwa cha kujitegemea kwa zaidi ya asilimia 74, jambo linalohitaji umakini mkubwa katika ukusanyaji wa mapato na udhibiti wa matumizi. Amesema Tanzania inapaswa kujiandaa kukabiliana na changamoto za kiuchumi zinazoweza kujitokeza kadri Nchi inavyoendelea kujitegemea zaidi kifedha, huku akisisitiza umuhimu wa uwajibikaji kwa watendaji wa Serikali. Bulaya pia amepongeza hatua ya Serikali kuondoa baadhi ya tozo kwa magari yanayotumia gesi na umeme ili kuhamasisha matumizi ya nishati mbadala, lakini akaitaka kwenda hatua zaidi kwa kupunguza matumizi ya magari yenye gharama kubwa za mafuta katika taasisi za umma. โ€œTuondoe matumizi ya magari yanayotumia bajeti kubwa kwenye mafuta ili fedha ziende kwenye miradi ya maendeleo,โ€ amesema Bulaya. โ€œHivi mimi najiuliza Mtu sio Mkurugenzi wa Taasisi wa maeneo mbalimbali hivi anatumia V8 ya nini ambazo zinatumia gharama kubwa kwenye mafuta, twende tukaondoe na matumizi ya magari yanayotumia bajeti kubwa kwenye mafuta ili pesa ziende kwenye miradi ya maendeleo,โ€ #MillardAyoUPDATES

millardayo

16,944 ๆฌก่ง‚็œ‹ โ€ข 1 ไธชๆœˆๅ‰

Mbunge wa Buchosa, Eric Shigongo amesema Serikali ya Tanzania au ya Nchi yoyote Duniani inapokopa kwa ajili ya maendeleo sio jambo baya kwasababu Nchi zote Duniani ikiwemo Marekani zinakopa huku akisema Tanzania ni miongoni mwa Nchi zenye madeni madogo kuliko Nchi nyingi za Afrika ambapo amemsifu Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jinsi anavyoendelea kuimairisha uchumi. Akiongea na Waandishi wa Habari Jijini Dar es salaam, Shigongo amesema โ€œMimi nakopa ni Mtu mmoja na Nchi zote zinakopa, Marekani hapo ilipo inadaiwa Trilioni 320 na China, Taifa kubwa Marekani wote mnaijua lakini inakopa China, juzi nilikuwa na Seneta mmoja ananiambia โ€˜sisi tumekopa Trilioni 333 kutoka China, tukizileta hapa tunazipeleka Afrika sisi tunabaki na deniโ€™, hii inaonesha kukopa kwa ajili ya maendeleo sio kitu kibayaโ€ โ€œSerikali inapokopa sio jambo baya kwasababu Nchi zote Duniani zinakopa, na kwa taarifa yetu na Mimi nikiwepo Tanzania ni miongoni mwa Nchi zenye madeni madogo kuliko Nchi nyingi za Afrika, sisi tuna 38% ya uwezo wa kukopa ukilinganisha na kipato chetu, kwahiyo sisi nafasi yetu ya kukopa bado ni kubwa, na Mimi nashauri kama tutahitaji kukopa ili tujenge miundombinu ya umwagiliaji Nchi nzima, tukope, kwasababu ndio Dunia inapokwenda, ila tukope mikopo yenye masharti nafuu, kwahiyo Mimi sio madharaโ€ โ€œWatanzani wenzangu nawaomba tunapotaka kukopa kwa ajili ya maendeleo tusisite kukopa kwasababu ndio Dunia inavyoendeshwa, ombi langu kama Nchi tusiogope kukopa pale inapotakiwa kufanya hivyo kwa ajili ya maendeleo yetu, jambo muhimu kufanya ni kuhakikisha mikopo inapokuja kuwe na uadilifuโ€ #MillardAyoUPDATES

millardayo

38,428 ๆฌก่ง‚็œ‹ โ€ข 1 ๅนดๅ‰

Kwa msiojua anachosema huyu mwana wa wana mtandao โ€” Ikuluu imeomba kutumia Trilion 1.5 โ€” Fedha kwa matumizi ya kawaida trilioni moja hii ni kwa ajili ya ulinzi , TISS NA SAFARI za Raisi pamoja na nguo na chai za Ikulu hayo ndio uwa matumizi ya kawaida , mishahara ya watu wa ikulu na TISS, hii pesa yote haikaguliwi na CAG ni ya Iddi Amin mama kugawana na washikaji wake โ€” Pia inatumika kwenye matukio na sherehe za Ikulu iko kwenye hiyo trilion pia haikaguliwi na CAG kwa kifupi hiyo Trilion ni pesa ya mfukoni ya Samia kwa maana nyingine hiyo Trillion moja ndio sadaka tumetoa kwa maisha ya Samia Ikulu na wenzake โ€” Wameomba pia billion 500 kwa matumizi ya maendeleo, Hii inakwenda kwenye ukarabati wa Ikulu , kununua mapazia , magari , kununua siraha za TISS na uniform, kujenga Ikulu au chochote hapo ikulu , kununu furniture za ndani , kununua mapambo ya Ikulu Hii pia haikaguliwi na CAG uwezi thibitisha imetumikaje Fedha yote hii inazidi matumizi ya wilaya ya Afya , inadizi matumizi ya bodi ya mikopo kwa wanafunzi nchi nzima Inazidi mbali bajeti ya kilimo nchi nzima , inalingana na matumizi ya Wizara ya ujenzi inakaribiana na bajeti ya nchi nzima ya Jeshi lote Inazidi matumizi ya polisi , inazidi bajeti ya maji nchi nzima Ndio maana tunataka katiba mpya Hatuitaji trilioni 1.5 isiyokaguliwa kwa usawa huu, ambayo ni pelemende kwa mtu mmoja Machawa wote wanalipwa na hii bajeti Hii ni bajeti pekee utekelezwa kwa 100% yaani pesa yote inapatikana na kupelekwa IKULU , hizo bajeti nyingine uwa zinatekelezwa kwa 40% or chini kuna ambazo uwa wanasoma lakini mwisho wa siku wanapeleka pesa 35% na ndio maana unasikia kama barabara wanasema Barabara moja hata kwa miaka 4 sababu bajeti haikutekelezwa kwa 100% Lakini hii ya IKULU uwa wanapelekewa pesa kwenye malori kutoka BoT kisha wanaanza tumia watakavyo Hakuna pesa ya bure dunia kama hii, kuna wakati Kikwete akiwa Raisi Ikulu ilinunua mapazi ya million 300 ikavuja na kuleta maneno Kuna hizo saa na pete za millioni 400 anazofaa Samia zinatoka kwenye hii bajeti Kuna nguo hizo mnaona anavaa za mabilioni zinatoka kwenye hii bajeti Kwa ukubwa wa TISS na kwa namna ambayo tayari imeshawekezwa hata kutumia billion 500 ni nyingi sana Hii ndio pesa mara furani Samia amekwenda na wasanii Korea wakafanyia shopping mabegi mawili yamejaa kila msanii na kupewa pesa ndefu Ndio pesa pia ilitumika marekani kufunga Hotel mbili zimejaa machawa na wasanii wakiwemo waandishi wa habari ikaleta gumzo kubwa

Think Different

28,461 ๆฌก่ง‚็œ‹ โ€ข 3 ไธชๆœˆๅ‰

Mbunge wa Jimbo la Ikungi Magharibi, Elibariki Kingu ameishauri Serikali kuanzisha mfumo wa kuchangia Bima ya Afya kwa wote kupitia miamala ya simu, ambapo kila Mtanzania angechangia kiasi kidogo cha fedha katika kila muamala anaoufanya. Akichangia Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2026/27, May 11, 2026, Bungeni Jijini Dodoma, Kingu amesema Tanzania ina idadi kubwa ya miamala ya simu inayoweza kutumika kama chanzo cha uhakika cha kugharamia huduma za afya bila kuongeza mzigo mkubwa kwa Wananchi. โ€œNimefanya statistics kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania na kusoma ripoti za Benki Kuu ya Tanzania, Tanzania kwa mwaka mmoja inarekodi miamala bilioni 6.3 kwa Watu wanaofanya miamala kwenye mitandao ya simu na miamala mingine, Mchengerwa mnasubiri nini kuja na platform kwenye hii Nchi, sio mkalete tozo mpya zitakazowapa Watanzania mzigo, mimi nawapa mawazo, njooni na โ€˜coding systemโ€™ ambayo itatumia teknolojia ya kisasa Watanzania wako tayari kuchangia Bima ya Afya kwa wote, wanachosubiri ni kupewa mwelekeo,โ€ amesema Elibariki Kingu. Aidha amesisitiza kuwa hata mchango mdogo wa shilingi 10 au 30 kwa kila muamala unaweza kusaidia Serikali kukusanya fedha nyingi zitakazowezesha Wananchi kupata huduma bora za afya bila kuambiwa kwenda kununua dawa nje ya Hospitali. โ€œKwa hesabu hizi mnaweza mkakusanya trilioni nne mkafadhili Bima ya Afya kwa wote Watanzania wakienda Hospitali wasiambiwe dawa nenda kanunue kwa Mtu fulani,โ€ amesema Elibariki Kingu. #MillardAyoUPDATES

millardayo

27,433 ๆฌก่ง‚็œ‹ โ€ข 2 ไธชๆœˆๅ‰

Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameitaka Wizara ya Mambo ya Nje, Wizara ya Mambo ya Ndani na Vyombo vya Ulinzi na Usalama kuchukua hatua za haraka kwa wanaotumia mitandao na teknolojia vibaya, akikemea pia wingi wa Wanaharakati kutoka nje ya nchi wanaojaribu kuingilia mambo ya ndani ya Tanzania na kutaka kuivuruga amani. Rais Samia amesema hayo Jijini Dar es salam leo May 19, 2025 wakati akizindua Sera ya Mambo ya Nje ya Mwaka 2001 (Toleo la 2024), ambapo amesema hatotoa nafasi kwa watovu wa adabu kutoka nje ya nchi kuja kujaribu kuvuruga amani, utulivu na usalama uliopo nchini Tanzania. โ€œTusiwe shamba la Bibi kwamba Mtu anaweza kuja Tanzania akasema analolitaka, lipo Tanzania halipo, Watu wakajisemea tu, tumeanza kuona mwenendo wa Wanaharakati ndani ya Ukanda huu kuanza kuvamia na kuingilia mambo yetu huku, sasa kama kwao wameshadhibitiwa wasije kutuharibia, tusitoe nafasi walishavuruga kwao, nchi iliyobaki haijaharibika ni hapa kwetu, niwaombe Vyombo vya Ulinzi na Usalama kutotoa nafasi kwa Watovu wa adabu wa nchi nyingine kuja kutovuka hapa kwetu, hapanaโ€ โ€œNimeona clip kadhaa za kunisema, nipo bias na nini, ninalofanya ni kulinda nchi yangu na ndiyo wajibu wangu niliopewa, kwahiyo hatutotoa nafasi kwa kiumbe yeyote kuja kutuvurugia hapa awe yupo ndani ama anayetoka njeโ€ Katika maelezo yake, Rais Samia ameitaka Wizara na Maafisa wanaohusika kutoa ufafanuzi kuhusu yale yanayosemwa na Wanaharakati na Watu mbalimbali, kukanusha ama kuchukua hatua za haraka ikiwa yanayosemwa yana ukweli kuhusiana na sekta zao mbalimbali. #MillardAyoUPDATES

millardayo

32,258 ๆฌก่ง‚็œ‹ โ€ข 1 ๅนดๅ‰