
(---) Onesmo Mushi
@EduTalkTz • 43,666 subscribers
Power tends to corrupt, and absolute power corrupts absolutely — Lord Acton
Shorts
Videos

Mhaini anaongea kwenye vyombo vya habari na serikali inamwangalia tu?😎😎😎 Hii nchi hii🙌🏿🙌🏿🙌🏿🙌🏿!!
(---) Onesmo Mushi86,941 просмотров • 11 дней назад

Ukiwa mlevi au mjinga, utamlaumu konda na kusahau kuwa hii ni biashara yake. Kama ambavyo wewe hauwezi kutoa mchele wa bure dukani kwako, ndivyo ilivyo kwa biashara ya usafirishaji. Ukiwa na akili timamu utalaumu watu uliowaweka madarakani. Wakati kwenye nchi za wenzetu serikali zinanunua na kuoperate mabasi ya shule kuhakikisha watoto wanafika mashuleni na kurudi nyumbani kwa wakati, viongozi wa Tanzania wanatumia trillion moja kugharamia safari zao za anasa. Pesa ya mabasi ya shule ndio hiyo wanatumbua nayo starehe; ndio yale mabilioni wanauolipa wabunge; ndio yale mabilioni ya kukimbiza mwenge, and the list goes on and on.
(---) Onesmo Mushi17,996 просмотров • 6 дней назад

Kwa hiyo mlimbambikizia kesi ya KUNYONGWA halafu hamtaki ANYONGWE?🤔🤔🤔 Mbona hamueleweki?
(---) Onesmo Mushi41,096 просмотров • 18 дней назад

Baada ya kusema haya, jamaa wameamua kumkamata Madeleka. Usishangae kesho ukiambiwa “alikuwa gaidi.”
(---) Onesmo Mushi47,529 просмотров • 28 дней назад

Mtaka ni mbegu nzuri iliyoanguka kwenye udongo mbaya. Kuna mambo hauwezi kufake, ni ama unayo au hauna. Ameuliza swali muhimu sana ambalo Mwal. Richard Mabala amekuwa akisisitiza kila mara anaposema “Mungu pekee ndio mwenye uwezo wa kusema iwe ikawa.” Huu “uchumi wa dola trillion moja” by 2050 unatengenezwa na human resource ipi? Mtoto anayezaliwa leo hii ana mazingira yoyote ya kumwandaa kushiriki kikamilifu kwenye uchumi, tofauti na mama yake aliyezaliwa miaka 15 - 20 iliyopita? Ni kipi haswa kilichobadilika kwenye elimu ya Tanzania ambacho unaweza kusema “hawa wa jana hakika hawakuandaliwa lakini hawa wa leo wana uhakika wa kuwa rasilimali watu?” JIBU LA MSINGI NI HAKUNA. Mazingira ni yale yale, miundombinu duni ni ile ile, tatizo la walimu ni lile lile, vifaa vya TEHAMA ni changamoto vile vile, na bajeti ni kiduchu vile vile. Tena kama haitoshi ndio kwanza tumeongeza idadi ya wanafunzi mara dufu halafu juu yake tukakopi sehemu ya sera ya elimu ya Finland na kuitumbukiza Tanzania. Mwanafunzi mzuri wa policy borrowing anaweza kutabiri with certainty kuwa tulichofanya ni mbili jumlisha mbili toa nne, haswa kwa kuzingatia uhalisia wetu wa kimiundombinu. Hoja nyingine nyeti ni hii ya KUSUBIRI KUSAIDIWA KILA KITU. Yani hata kutumia wataalam wetu kama wakina Kipanya na Mabala kututengenezea makala za kufundishia imekuwa changamoto, mpaka tusubiri “WAHISANI.” Pata picha hadithi za ucheshi wa kufundishia za Mabala, ambaye ni mtaalam wa literacy, zimekutana na katuni za Kipanya, vyote kwenye program moja. Ameuliza Mtaka, ni kipi haswa kwenye katuni ya Akili and Me kinachohitaji mtu kutoka nje?? Mwisho Mtaka akagusa panapouma. Katuni za HakiElimu kuhusu uhalisia wa mazingira ya kufundishia zilikuwa na shida gani?? Hatutaki kuambiwa ukweli kuhusu hali ya madawati mashuleni, vyoo, changamoto kubwa ya walimu na uwezo wao, pepo la lugha ya kufundishia n.k. Kila mara jamaa wakidepict uhalisia, mnasema “oohhhh wanashusha moral ya walimu; ooohhh wanamdharaulisha mwalimu; ooohhh wanaondoa utu wa wanafunzi; ooohhhh blah blah blah.” Tunapenda political correctness kiasi kwamba tupo tayari kuficha ukweli na kuacha watoto waendelee kusomea kwenye mazingira ya tabu na mateso kuliko kukabiliana na ukweli.
(---) Onesmo Mushi27,251 просмотров • 29 дней назад

“NO PREBLEM.”😂😂😂😂 Arena ifo nsuti k’mamayo😂😂😂😂!
(---) Onesmo Mushi42,679 просмотров • 2 месяцев назад

Walimu wengi sana Tanzania huwa tunatumbukia kwenye hili shimo. Mtu ana mshahara wa laki sijui saba nane, anakopa milioni 20 15 CRDB, NMB, etc., halafu anaitumbukiza kwenye ujenzi. Baada ya hapo hana mshahara wala nyumba, kinachoendelea Mungu ndio anajua.
(---) Onesmo Mushi27,295 просмотров • 1 месяц назад

Mwalimu Richard Mabala , mchukue ndugu yako mzungumze kinyumbani bhana😎.
(---) Onesmo Mushi22,685 просмотров • 1 месяц назад

Kwenye Riwaya ya Crime and Punishment, Fyodor Dostoevsky anazungumzia namna NAFSI inavyoweza kumwadhibu yule anayetenda uovu kuliko hata jela. Anasema unaweza kufake kwa tabasamu na ngonjera za hapa na pale lakini nafsi itakutandika mpaka uteme moto. Hii ni kwa muuwaji, sijui hali ipoje kwa yule ambaye analazimika kuficha siri za muuwaji na kuutetea uuwaji. A must read kwa wakati huu!!
(---) Onesmo Mushi10,716 просмотров • 15 дней назад

Tanzania kitendo cha kusema tu “hupendi nini kuhusu Rais” tayari kinatosha kukupoteza.
(---) Onesmo Mushi18,203 просмотров • 1 месяц назад

Ndio utapeli unaofanywa na wanasiasa wa Tanzania, kila kitu ujanja ujanja. Elimu ya juu imegeuzwa kuwa tissue paper, inapangusa upumbavu wa watawala tu. Chukulia mfano Mwigulu Nchemba. Wakati anafanya PhD pale UDSM 2012 - 2017, alikuwa pia Mbunge anayehudhuria vikao vya Bunge Dodoma, Mjumbe wa Kamati za Bunge za Bajeti, Katibu wa NEC wa Uchumi na Fedha, Mhazini wa CCM, Naibu Waziri wa Fedha, Waziri wa Kilimo, na Waziri wa Mambo ya Ndani. Chuo Kikuu cha Daresalaam University of Doha for Science and Technology kinatuaminisha kwamba wakati Mwigulu Nchemba anatekeleza majukumu yote haya aliweza pia kupata muda wa kujiandikisha kama mwanafunzi wa PhD full time. Yani wakati anatekeleza majukumu yote haya, aliweza pia kuhudhuria vipindi vyote na kukamilisha coursework, akapata muda wa kufanya tafiti, kuchapisha makala, kuandika dissertation, halafu kama haitoshi, akamaliza yote haya ndani ya miaka mitano na kutunukiwa PhD. Unless haufahamu what it takes kufanya PhD, huu ni muujiza wa hali ya juu. Hata hivyo haishangazi kwa sababu ni UDSM hii hii ailiyompa Samia PhD ya heshima mara baada tu ya kuingia madarakani.
(---) Onesmo Mushi27,736 просмотров • 1 месяц назад

Mshunuzi Christian Bwaya eehh, unaona sasa ni kwa nini huwa tunalazimika kuhoji elimu za hawa watu?
(---) Onesmo Mushi18,186 просмотров • 1 месяц назад