Jambo TV's banner
Jambo TV's profile picture

Jambo TV

@Jambotv_959,421 subscribers

Independent News Source | WhatsApp+255767252999

Shorts

Tupate wadhamini kidogo kabla ya kwenda kula biriyani pale kwa Shilole #ShishiFood

Tupate wadhamini kidogo kabla ya kwenda kula biriyani pale kwa Shilole #ShishiFood

71,943 Aufrufe

Videos

Jambotv_'s profile picture

VIDEO: Kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Joseph Selasini amekiasa chama hicho kutumia vyombo vyake vya ndani kufanya uchunguzi wa tuhuma za kifedha ili kuwasafisha viongozi na kuimarisha imani ya wanachama wake. Akizungumza hivi karibuni kutokana na tuhuma za ubadhirifu dhidi ya Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA bara, John Heche ambazo zimekuwa zikitolewa na baadhi ya wanachama na viongozi mbalimbali wa chama hicho ambao wengine wamesimamishwa na uongozi wa CHADEMA kwa kuhoji suala hilo, Selasini amesisitiza kuwa vyama vya upinzani vinapaswa kuwa tofauti na CCM kwa kile alichokiita kuficha mambo. Amedai kuwa upinzani unaikosoa CCM kwa kuficha mambo, hivyo ni lazima wao waoneshe mfano kwa kuwa wawazi zaidi katika taratibu zao. “Ninachosema tu ni kwamba tumemsikia Katibu Mkuu na kwasababu chama chetu ni chama cha kidemokrasia ni matumaini yangu kwamba hilo jambo litawekwa wazi zaidi kwa maana kwamba chama kina vyombo. Sasa kama kina vyombo ili kuwa-contain wanachama, kuwaleta wanachama pamoja, kuleta ule uaminifu wa pamoja ni vizuri vile vyombo vikafanya kazi yake na kazi ikiwa nzuri maana yake viongozi wanasafishika”, ameeleza Selasini”, ameeleza Selasini. Hata hivyo, akizungumza na wanahabari Julai 10, 2026, Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika alisema kama kuna mwanachama yeyote wa chama hicho ambaye ana taarifa zozote za malalamiko anapaswa kufuata taratibu za kikatiba za chama hicho na Zaidi akaeleza kuwa walikuwa na taarifa kuwa wale ambao wamekuwa wakitoa tuhuma dhidi ya viongozi wamekuwa wakilipwa fedha mpaka milioni mbili kwa lengo la kuchafua viongozi.

Jambo TV

104,753 Aufrufe • vor 15 Tagen