
Jamii Forums
@JamiiForums • 1,840,353 subscribers
Inform | Engage | Empower | Digital Democracy
Shorts
Videos

Mdau aliyejitambulisha kuwa ni Mwanafunzi wa Uhandisi Vifaa Tiba (Biomedical Engineering) ametoa wito kwa mamlaka zinazohusika kuangalia utaratibu wa Wanachuo kutakiwa kulipia ili kupata nafasi ya mafunzo ya vitendo (field practice) katika baadhi ya taasisi kubwa akitolea mfano hospitali. Yapi maoni yako Mdau? Fuatilia Mjadala #JamiiForums #JFMdau2026 #Uwajibikaji Video credit: maria_robyt
Jamii Forums30,714 Aufrufe • vor 3 Tagen

Waziri Deogratius Ndejembi ametoa maelekezo hayo, Juni 28, 2026, Ubungo jijini Dar es Salaam katika Kituo cha usimamizi wa Gridi ya Taifa ambapo ametaka kamati hiyo ishirikishe wataalamu kutoka Wizara ya Nishati, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) pamoja na Vyombo vya Ulinzi na Usalama. Fuatilia zaidi #JamiiForums #Uwajibikaji
Jamii Forums25,975 Aufrufe • vor 6 Tagen

KUMBUKIZI: Masanja Kadogosa, ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Bariadi Vijijini aliyasema hayo Februari 26, 2024, alipokuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), akizungumza na Waandishi wa Habari kabla ya kuanza kwa safari ya majaribio ya treni ya umeme ya abiria kutoka Dar es Salaam kuelekea mjini Morogoro. Zaidi tembelea #JamiiForums #Uwajibikaji #ServiceDelivery
Jamii Forums21,028 Aufrufe • vor 6 Tagen

DAR: Mchambuzi wa Siasa, Paternus Niyegira ameyasema hayo Juni 26, 2026 alipokuwa akihojiwa Crown FM, ambapo alizungumzia maelekezo ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi kuhusu zuio la mikutano ya Vyama vya Siasa nchini. Fuatilia zaidi👉🏽 #JamiiForums #Uwajibikaji #Utawala
Jamii Forums15,460 Aufrufe • vor 5 Tagen

PWANI: Baadhi ya Wananchi waliojitambulisha kuwa ni Wakazi wa Kisarawe wamedai kudhalilishwa na kuvunjiwa milango na Askari waliovamia makazi yao usiku bila kufuata utaratibu wa Kisheria. Pia, wamedai Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Petro Magoti, ndiye aliyewatuma Watu hao kufanya uvamizi. Kuhusu madai hayo DC Magoti amesema, “Mimi sina maelezo yoyote ndugu yangu nashangaa hii clip na mpaka sasa sielewi chochote.” Fuatilia zaidi #JamiiForums #Uwajibikaji #JFMatukio
Jamii Forums23,950 Aufrufe • vor 12 Tagen

TANGA: Waziri wa Mambo ya Ndani, Patrobas Katambi ameyasema hayo wakati wa hafla ya kufunga Mafunzo ya Awali, Kozi Na.6/2026 katika Chuo Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Chogo, Wilayani Handeni ambapo askari 1,000 wamehitimu mafunzo hayo. Zaidi tembelea #JamiiForums #Demokrasia
Jamii Forums12,304 Aufrufe • vor 10 Tagen

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT), Sheikh Alhad Mussa Salum ameyasema hayo Jumanne, Mei 26, 2026, alipokuwa akizungumza na Waandishi wa Habari katika mkutano ulioandaliwa na JMAT jijini Dodoma. Kauli hii inakuja siku chache baada ya Maseneta wawili wa Marekani, Jeanne Shaheen na Ted Cruz, kuwasilisha muswada katika Seneti ya Marekani uliotaka Serikali ya Marekani kufanya tathmini ya mahusiano yake na Tanzania. Zaidi tembelea #JamiiForums #Diplomasia #JFDiplomacy
Jamii Forums36,571 Aufrufe • vor 1 Monat

ZANZIBAR: Naibu Waziri wa Vijana, Ajira na Uwezeshaji Hassan Khamis Hafidh amesema hayo Juni 6, 2026 katika Baraza la Wawakilishi Zanzibar, wakati akichangia Makadirio ya Mapato na Matumizi Bajeti ya Vijana. Nini maoni yako Mdau? Shiriki mjadala #JamiiForums #Utawala
Jamii Forums21,163 Aufrufe • vor 26 Tagen

DAR: Mchora Katuni ambaye pia amewahi kuwa Mtangazaji wa Redio na TV, Masoud Kipanya ametoa kauli hiyo Mei 15, 2026 akieleza mtazamo wake kuhusu Waandishi wa Habari walioshiriki kuwania nafasi za uongozi kupitia Vyama vya Siasa. Je, Uhuru wa Habari utakuwa hatiani kulingana na mgongano huo wa kimaslahi? Nini maoni yako Mdau? Zaidi bofya #JamiiForums #Uwajibikaji #Siasa Video: Tell A Vision
Jamii Forums33,349 Aufrufe • vor 1 Monat

DAR: Ally Mkii amefungua shtaka la Madai Mahakama Kuu, akiitaka Hospitali ya Aga Khan imlipe fidia ya Tsh. Bilioni 1.2, akidai uzembe wa kimatibabu umesababisha Mtoto wake akatwe mguu alipofika hapo kutibiwa Wakili wa Ally, Pasensa Kurubone, amesema Washtakiwa ni Hospitali hiyo na Daktari aliyehusika, ambapo Mahakama imetupilia mbali pingamizi la Hospitali lililotaka shauri lisikilizwe na Mabaraza ya Waganga Upande wa Ally Mkii amesema “Tulimpeleka Aga Khan Tawi la Mbagala, Mwaka 2022, baada ya vipimo tukapelekwa Aga Khan ya Mjini, wakasema ana mvunjiko mdogo, akafungwa POP. Ikatakiwa turudi baada ya Wiki 3, hali ikawa mbaya tukarudi baada ya Wiki, ikabainika POP imebana na kushindwa kupitisha Damu” JamiiForums imewasiliana na Meneja Masoko na Mawasiliano wa Aga Khan, Olayce Lotha aliyesema “Suala lipo chini ya Mkurugenzi wa Tiba na Afya pamoja na Wanasheria wetu, nalielekeza kwao kwa taarifa na ufafanuzi zaidi.” Soma #JamiiForums #Accountability
Jamii Forums217,969 Aufrufe • vor 1 Jahr

SIASA: Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amesema Mwaka huu (2024) Serikali haitapeleka Huduma ya Dawa, Mbegu wala Wanunuzi kwenye Jimbo la Kisesa kwa kuwa Mbunge wao (Luhaga Mpina) amekuwa akisema Serikali inapeleka huduma feki Bashe ameongeza kwa kusema kuwa atakwenda Kisesa kuwauliza Wananchi ili kama hayo ni mawazo yao huduma hizo zitasitishwa ili Wananchi na Mpina wasimamie suala hilo Soma #JFMatukio #Governance #JamiiForums
Jamii Forums280,852 Aufrufe • vor 1 Jahr

DAR: Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar limesema linawashikilia Watu 8 kwa tuhuma za tukio la Novemba 11, 2024 eneo la Kiluvya ambapo Watu kadhaa walifanya jaribio la kumteka Mfanyabiashara, Deogratius Tarimo, Mkazi wa Kibaha - Pwani Kamanda Kanda Maalum ya Polisi, Muliro J. Muliro - SACP amesema Watuhumiwa wamekamatwa kwa nyakati tofauti katika Mikoa ya Dar, Songea Ruvuma na eneo la Mbingu Mlimba Morogoro, pia wamekamata gari aina ya Toyota Raum waliyoitumia wakati wa tukio ikiwa na namba T 237 EGE ambayo si halisi, ambapo uchunguzi umebaini namba halisi ni T237 ECF Amewataja waliokamatwa kuwa ni Bato Bahati Tweve (umri Miaka 32 – Bondia), Yusuph Abdallah (32), Fredrick Juma (31), Nelson Elimusa Msela (24 - Dereva Tax), Benk Daniel Mwakalebela ‘Tall’ (40), Thomas Ephraim Mwakagile ‘Baba Mage’ (45), Anitha Alfred Temba (27) na Isack Mwaifani (Bondia) Soma #JFMatukio #JamiiForums #Accountability
Jamii Forums221,810 Aufrufe • vor 1 Jahr

DAR: Dereva wa Mabasi Yaendayo Haraka (Mwendokasi) ambaye jina lake halijafahamika, akiendesha kutoka kituo cha Gerezani kwenda Kimara, amedaiwa kutosimama kwenye vituo vingi vya njiani baada ya kurushiana maneno na Abiria ambao walilalamikia uendeshaji wake Mdau wa amedai licha ya Basi kujaa, Dereva aliendelea kupakia Abiria ambapo walilalamika kuwa anawaumiza kwa kufungua na kufunga milango, hali iliyoibua ubishani. Baada ya kutoka Kituo cha Magomeni Dereva hakusimama, akawapeleka Abiria wote Kituo cha Kimara Mwisho Anadai walipofika Kimara, Dereva alishuka na kuondoka na baada ya mvutano wa muda mrefu, Dereva mwingine akaamua kuchukua basi husika na kuwarejesha wale waliopitilizwa vituo Soma #JFHuduma #JFUwajibikaji #JamiiForums
Jamii Forums298,633 Aufrufe • vor 2 Jahren

DAR: Uongozi wa Serikali ya Mtaa wa Oysterbay ukiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama umewatia mbaroni raia wa kigeni wenye asili ya Kichina wakiwa na kiasi cha takriban Tsh. Bilioni 6 taslimu zilizokuwa zimefichwa katika "Apartment" Namba 317, ghorofa ya tatu, Jengo la Phoenix, Mtaa wa Mazengo. Aidha, Afisa Uhusiano wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Doreen Kapwani amesema “Kesho (Januari 7, 2026) ufafanuzi kamili utatolewa kuhusu tukio hilo kupitia kwa Kamanda wa Polisi Kinondoni. TAKUKURU tulikuwepo na tumeshiriki.” Soma #JamiiForums #Accountability #KemeaRushwa #JFMatukio
Jamii Forums80,102 Aufrufe • vor 5 Monaten