
EastAfricaTV
@eastafricatv • 2,060,873 subscribers
Official EastAfricaTV (EATV) Twitter Email: [email protected]
Shorts
Videos

#HABARI Waziri wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, amesema Katiba Mpya inayohitajika nchini inapaswa kulenga kutatua changamoto za wananchi, badala ya kuwa chombo cha baadhi ya viongozi kugawana madaraka. Akizungumza Julai 10 wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa Kituo cha Polisi Ussoke, wilayani Urambo mkoani Tabora, Ridhiwani aliwataka wananchi, hususan vijana, kupuuza wito wa maandamano unaotolewa mitandaoni, akisema baadhi ya wanaohamasisha hawakushiriki kukusanya maoni ya wananchi. Amesema Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inaelekeza mchakato wa Katiba Mpya kufanyika ndani ya miaka mitano ijayo kwa kuzingatia maoni ya wananchi na kufuata utaratibu, badala ya shinikizo au vurugu. #EastAfricaTv
EastAfricaTV18,694 views • 2 days ago

#VIDEO Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Mwanga, Mkoa wa Kilimanjaro na Mjumbe wa Baraza Kuu la Taifa la chama hicho, Lembrus Mchome, amepinga kauli zinazodai kuwa baadhi ya wanachama wanaokosoa mwenendo wa chama hicho wanalipwa fedha ili kukichafua, akisema madai hayo hayana msingi na yanapaswa kupuuzwa. Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumamosi Julai 11, 2026, Mchome amesema wanaopigania Katiba ya CHADEMA wanafanya hivyo kwa mujibu wa misingi ya chama, huku akisisitiza kuwa Katiba inaruhusu wanachama kukosoa pale wanapoona kuna changamoto au mwenendo usio sahihi ndani ya taasisi hiyo. “Katiba ipo wazi na imeturuhusu kupinga uovu wowote unaofanyika. Mnyika akisema tunalipwa najaribu kuwaza, wakati ule Tundu Lissu akiwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA alisema kuna fedha chafu ndani ya CHADEMA, je alikuwa analipwa na CCM? Na Makamu Mwenyekiti wa sasa John Heche mwaka 2024 aliposema ndani ya CHADEMA kulikuwa na fedha chafu, naye alikuwa analipwa na nani." Amesema Mchome. #EastAfricaTV
EastAfricaTV17,629 views • 2 days ago

#HABARI Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida linamtafuta mtuhumiwa anayejulikana kwa jina la Kasimu Ally Juma (34), mkulima na mkazi wa Kinyankaya, Kata ya Unyambwa, Wilaya ya Singida, kwa tuhuma za kupandisha bendera tano zinazofanana na Bendera ya Taifa la Tanzania katika shamba lake. Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida SACP. Amon Kakwale, amesema tukio hilo lilibainika Juni 26, 2026 majira ya saa 5:00 usiku baada ya Polisi kupata taarifa kutoka kwa wananchi. Uchunguzi wa awali ulibaini uwepo wa bendera hizo pamoja na bango lenye ujumbe unaosema “UZINDUZI WA MAPENZI.” Mtuhumiwa alitoroka baada ya kubaini kuwa anafuatiliwa na Jeshi la Polisi. Upekuzi uliofanyika nyumbani kwake ulifanikiwa kukamata baadhi ya vifaa vinavyosadikika kutumika kutengeneza bendera hizo. Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida linaendelea na juhudi za kumtafuta mtuhumiwa huyo na linawaomba wananchi kutoa taarifa zitakazosaidia kupatikana kwake. #EastAfricaTV
EastAfricaTV51,077 views • 1 month ago

#Bungeni: Akichangia Bajeti ya Wizara ya Elimu, Mbunge wa Kuteuliwa (CCM), Shamsi Vuai Nahodha ameweka mkazo kwenye uhusiano wa kile kinachofundishwa darasani na uhalisia wa maisha. Kwa urefu zaidi unaweza kuitazama kupitia YouTube channel yetu ya EastAfricaTV #EastAfricaTV #Bungeni #HainaKuchoka #EATV2025
EastAfricaTV223,690 views • 1 year ago

#HABARI Rais wa Chama cha Mawakili Tanganyika Boniface Mwabukusi, amemkosoa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Patrobas Katambi (Mb) kwa kauli yake ya kutoa agizo kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Camilius Wambura la kuzuia mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa kote nchini akifafanua kwamba, Jeshi la Polisi ni Chombo kinachojitegemea na sio kitengo katika Wizara ya Mambo ya Ndani. #EastAfricaTV
EastAfricaTV12,768 views • 16 days ago

#HABARI Simanzi imetawala Mtaa wa Matindigani, Kata ya Pasua wilayani Moshi baada ya mtoto mwenye umri wa miaka sita, Idrisa Khatibu Ramadhani, aliyekuwa akitafutwa tangu jana, kukutwa amefariki ndani ya bwawa la kufugia samaki leo Mei 31, 2026. Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Kilimanjaro, Philbert Beda, amesema mtoto huyo alipatikana akiwa amefariki ndani ya bwawa hilo na kwamba uchunguzi wa chanzo cha tukio unaendelea. Baba wa marehemu, Khatibu Ramadhani, amesema familia ilikesha ikimtafuta mtoto huyo baada ya kutoweka jana jioni kabla ya taarifa za kupatikana kwake kutolewa leo asubuhi. Baadhi ya wananchi wa eneo hilo wameeleza kuwa bwawa hilo limekuwa hatari kwa muda mrefu kutokana na kukosa uzio imara, huku wakitaka lifukiwe ili kuzuia madhara zaidi kwa watoto. #EastAfricaTV
EastAfricaTV26,281 views • 1 month ago

#VIDEO Wafanyabiashara waofanya shughuli zao Mtaa wa Ally Maua A, Kijitonyama wameiomba Serikali iwasaidie kupunguza gharama za mabango kwani zimekuwa kubwa ukilinganisha na mzunguko wa biashara zao. EATV ikafika kwenye maduka hayo na kushuhudia aina za mabango na kiasi ambacho wametozwa. #EastAfricaTv #UtajiriWaHabari
EastAfricaTV237,457 views • 1 year ago

#VIDEO Huzuni imetawala Jijini Dodoma baada ya wanafunzi wawili wa chuo cha St.John's ambao ni Rebeca Misungwi na Felista Peter Fransis kufariki kwa ajali ya Moto uliotokea katika chumba walichokuwa wanaishi, huku Chanzo cha tukio la Moto huo ukihusishwa na Wivu wa Mapenzi Inaelezwa kuwa Moto huo uliwashwa na Mpenzi (Boy friend) wa mmoja ya wanafunzi hao (Felister) Boyfriend ambae pia ni Mwanafunzi wa Chuo kikuu hicho cha St John's Rebeca Misungwi alifariki dunia juzi tarehe 11 Juni, huku Felister amefariki dunia leo Juni 13 wakati akiendelea na matibabu katika Hosptali ya Kanda ya Benjamin Mkapa ya Jijini Dodoma Tukio la Moto huo, lilitokea usiku wa tarehe 6 na Mwili wa Rebeca umesafirishwa Jana kuelekea Wilaya ya Magu Jijini Mwanza kwa maziko #EastAfricaTV
EastAfricaTV18,188 views • 1 month ago

#VIDEO Wafanyabiashara Soko la Kariakoo, wameiomba Serikali kuwaondoa raia wa kigeni ambao wamekuwa wakiuza bidhaa rejareja kwa bei ya chini hali inayopelekea raia wa nchini kukosa wateja. Wakiongea na EATV, wanasema kwa sasa hali imekuwa mbaya zaidi kwani wengine wamekuwa wakisimama nje ya maduka na kuchukua namba za wateja na kuwapeleka kwenye maduka yao. #EastAfricaTv
EastAfricaTV211,497 views • 1 year ago

#VIDEO Bila kujua askari wa usalama barabarani katika eneo la Magugu wilayani Babati mkoani Manyara wameisimamisha gari ambayo ndani alikuwepo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa na kuikagua. Akizungumza na askari wa usalama barabara Waziri Bashungwa wakati akiwa safari mara baada ya kushudia askari hao wakitekeleza majukumu yao kwa weledi na uadilifu, amewasisitiza kuendelea kusimamia sharia za usalama barabarani ili kuepusha ajali ambazo kwa kiasi kikubwa husababishwa na uzembe wa madereva. “Nimeshamwambia IGP, barabarani sio machinjio ya watu, kwahiyo mnaposimamia majukumu yenu kwa weledi tunafurahi. Hakuna ambaye yupo juu ya sheria, mtu yeyote anayetumia chombo cha moto anapokuwa barabarani lazima azingatie sheria za usalama barabarani” Bashungwa akizungumza na Askari. #EastAfricaTV
EastAfricaTV194,404 views • 1 year ago

#VIDEO Jeshi la Polisi mkoa wa Njombe linamshikilia Baltazari Sonyonda(33) mkazi wa Iwungilo Halmashauri ya Mji Njombe kwa tuhuma za kusababisha mauaji ya Mariam Clalence Ndindile mwenye umri wa miaka 50 baada ya kumuingizia mkono sehemu ya haja kubwa mwanamke huyo na kisha kuuvuta utumbo na kuukata kipande na kukitoa nje. Akizungumza Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe, Mahmoud Banga, amesema chanzo cha tukio hilo ni wivu wa mapenzi, kwani mtuhumiwa alikuwa akimtaka mwanamke huyo kimapenzi na mwanamke huyo alikuwa akimzungusha mara kwa mara #EastAfricaTV
EastAfricaTV173,355 views • 1 year ago

#VIDEO Mlinzi Kanali Isaac Amponsah wa Rais wa Ghana anayemaliza muda wake Nana Akufo Ado, ameanguka siku ya jana Januari 03,2025, wakati Rais wa Ghana akisoma hotuba ya mwisho ya kuvunja Bunge na kuaga taifa, Mlinzi huyo, ameanguka katikati ya hotuba ya Rais, jambo lilofanya hotuba hiyo kusimama kwa muda kabla ya Rais Akufo kuendelea kuhutubia. Rais mpya wa Ghana John Mahama anategemewa kuingia rasmi madarakani mnamo Januari 07,2025, baada ya kuapishwa. Mahama aliyewahi kuwa Rais alitangazwa kuwa mshindi mnamo Disemba 2024, baada ya kumshinda mgombea wa chama tawala kwa asilimia 56.3 ya kura zote #EastAfricaTV
EastAfricaTV156,801 views • 1 year ago

Muigizaji na mfanyabiashara Jacqueline Wolper kwenye majukumu yake ya Mama akiwafundisha watoto wake Mitindo JR na Paris kuosha vyombo. Mashabiki wengi wamemsapoti baada ya kushea video wakielezea maoni yao juu ya malezi ya Wolper kwa watoto wake. #EastAfricaTV #TogetherTunawakilisha
EastAfricaTV20,737 views • 1 month ago

Video ya Madee akimtambulisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan ndani ya uwanja wa Emirates mbele ya mashabiki wa Arsenal. Madee anasema 🗣"Tunakila sababu kumsapoti @samia_suluhu_hassan haswa kwenye sekta ya michezo na tunaona juhudi zake anavopush michezo". "Kwa mara ya kwanza jana nimemtambulisha kwa mashabiki wa Arsenal na ameahidi kuanzia mechi ijayo kutakua na goli la Mama Arsenal ikifunga kama iliyvo 2025 Arsenal Bingwa basi hivyo hivyo 2025 Mama Bingwa". #RaisSamia #Madee #Arsenal #Emirates
EastAfricaTV123,858 views • 1 year ago