Mdude Nyagali's banner
Mdude Nyagali's profile picture

Mdude Nyagali

@mdudenyagali158,342 subscribers

Political Activist in Tanzania focusing on Civil Rights and Good Governance. 🇹🇿. #Author- #FiveYearsOfPain. - To buy my Book, please click the link below.

Shorts

Vibaka undercover kutoka polisi Police Force TZ wamefika Kariakoo kumkamata mtu wakiwa hawana sare za jeshi la polisi wala makosa wanayomtuhumu nayo. Wananchi wamegoma na kuwazingira askari hao wasiondoke mpaka aje OCS wa kituo jirani. Nasisitiza wakati mwingine wapigieni nduru ya weziii

Vibaka undercover kutoka polisi Police Force TZ wamefika Kariakoo kumkamata mtu wakiwa hawana sare za jeshi la polisi wala makosa wanayomtuhumu nayo. Wananchi wamegoma na kuwazingira askari hao wasiondoke mpaka aje OCS wa kituo jirani. Nasisitiza wakati mwingine wapigieni nduru ya weziii

88,790 Aufrufe

Videos

mdudenyagali's profile picture

7 x 70 Sumu ya Nyigu.

Mdude Nyagali

58,357 Aufrufe • vor 1 Jahr

mdudenyagali's profile picture

Huu ujumbe wa Zitto MwamiRuyagwa Kabwe tufanye tuwezavyo umfikie Samia Suluhu hata kwa njia ya WhatsApp. Nilishawahi kusema huko nyuma kwamba kwa sasa vyombo vya dola ndivyo vinavyoongoza siasa na sio siasa kuongoza vyombo vya dola. Huko nyuma vyama vya siasa ikiwemo ccm yenyewe vilikuwa na nguvu kuliko vyombo vya dola lakini kwa sasa vyombo vya dola ndio vina nguvu kuliko vyama vya siasa. Kwa sasa vyombo vya dola ndio vinapanga nani awe kiongozi ccm na 80% ya vyama vya upinzani. Vyombo vya dola vinaweza kumuondoa kiongozi yoyote kwenye vyama vya siasa wanavyoviendesha ikiwemo chama tawala na vingine kama walivyowaondoa akina Chongolo, Polepole, Kinana, Mbatia na wengine. Vyombo vya dola wanaweza kufanya hivyo kwa sababu wanamumdu Rais ambaye pia ni mwenyekiti wa chama tawala . Sasa vyombo vya dola ndivyo vinavyoamua nani awe mbunge au diwani wala sio wananchi tena wanaoamua. Yani kwa sasa kura za wananchi haziamui tena nani awe mbunge bali dola ndiyo inayoamua. Zamani ulikuwa ukisikia ccm wakijitapa kwamba ccm imeshika dola lakini kwa sasa dola ndiyo iliyoishika ccm. Kwamba kwa sasa ccm imebakia kama rubber stamp tu ya dola. Viongozi wa ccm hawana uhuru wa kutoa maoni na fikra zao kama zamani na wote wanalazimishwa kusifia tu serikali hata kama wakulima huko wamedhulumiwa na serikali. Muasisi wa hali hii ya kuifanya vyombo vya dola kuwa na nguvu kuliko siasa ni Magufuli na Samia amefanya kuiendeleza. Zitto amezungumza kitu cha kweli kama hali itaendelea kuwa hivi basi siku sio nyingi ccm wataondolewa na dola. Mdude Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.

Mdude Nyagali

52,990 Aufrufe • vor 1 Jahr

mdudenyagali's profile picture

Ikitokea tumepata serikali mpya nje ya chama cha mbogamboga jeshi la polisi lote linapaswa kufanyiwa overhaul. 1- Idara ya Field Force Unit - FFU ni ya kufuta kabisa waende nyumbani kwa sababu hawana kazi yoyote. Mara nyingi wanatumika vipindi vya uchaguzi kupiga mabomu na risasi na wakati mwingine kuvuruga mikutano ya upinzani. Baada ya hapo ni kurudi kambini kucheza draft na bao wakisubiri kipindi cha uchaguzi au mikutano ya upinzani wakapige mabomu. Yani askari zaidi ya elfu 15 wa FFU wanalipwa mshahara kwa ajili ya kazi hiyo tu. Hii ni hasara kwa taifa. Jambo lingine askari waliopo FFU ni adhabu baada ya kufanya makosa makubwa kwenye idara zingine za polisi. Kwa hiyo ukweli ni kwamba FFU yote imejaa vibaka waliopaswa kufukuzwa kazi kwa makosa mbalimbali waliyoyafanya kwenye idara zingine. Ndio maana unaona hawana nidhamu wala heshima na wanaendeshwa tu kama robot wanavunja watu miguu, kudhalilisha watu, kuwang'atisha mbwa watu na kuua watu kama walivyofanya majuzi pale Kisutu. Na walivyo bumunda utasikia inamisha vichwa chini msituangalie sura. Yani wanaamini kuwainamisha vichwa chini watu wanaowafanyia unyama ni salama kwao kutotambulika. Kumbe kutambulika ni suala la muda tu, mkibadilisha serikali anabanwa mkuu wakikosi analeta orodha ya askari wote waliohusika na oparesheni husika. 2 - Tunaweza kuanzisha idara mpya ya upelelezi nje ya polisi kama ilivyo FBI. Hii idara ya upelelezi inayojitegemea nje ya polisi tunaweza kuipa jina la Tanzania Top Bureau of Investigation - TTBI. Idara hii mpya haiitaji watumishi wengi. Inahitaji watumishi wasiozidi elfu 6 tu na wanahitaji ofisi moja kila mkoa na watumishi wasiozidi 300 kila mkoa. Zile Camp za FFU tunaweza kugeuza kuwa ofisi za idara hii. Kazi yao kubwa ni kila mkoa ni kufanya upelelezi wa makosa makubwa makubwa kama vile mauaji, human trafficking, ufisadi serikalini, ugaidi na mengine yanayofanana na hayo. Sare zao zinaweza kuwa nyeusi. Polisi wanaweza kubakia na upelelezi wa kesi ndogo ndogo kama wizi wa kuku, baiskel na vikesi vingine vya aina hiyo. Hii itasaidia kukomesha mateso na utekaji. Ukweli ni kwamba vikosi kazi Task force vinavyotumiwa kuteka watu vinaundwa na ma-RCO vina askari kanzu ambao mafunzo yao ya kufanya upelelezi ni madogo mno. Ndio maana hawana njia nyingine zaidi ya kupiga na kutoa mateso mengine kwa watuhumiwa wakiwalazimisha watoe majibu wanayotaka wao. Ikitokea mtuhumiwa ameamua kusema uongo ili kuwarilidhisha wasimpige basi wakigundua wamedanganywa humuua na kwenda kutupa mwili wake huko alikootwa SIR TIVA au mto Ruvu kwenye masalia ya mamba na maeneo mengine. Kumbe tunaweza kuwa na idara ambayo inaweza kufanya upelelezi na kukusanya ushahidi bila kuteka na kuua watu. Tukiwa na idara ya upelelezi ya viwango vya namna hii inaweza kupata sifa hadi nje ya nchi yetu. Kwamba waombaji wa nafasi za kazi wawe na fani mbalimbali zinazoweza kusaidia kufanya upelelezi mfano Cyber, udaktari, ukemia, sheria na fani zingine zinazoweza kusaidia upelelezi. Mafunzo yao yawe ya hali ya juu na vifaa vya kusaidia uchunguzi vya kisasa kabisa. Kwa hatua za kwanza tunaweza kutafuta wakufunzi FBI na mashirika mengine makubwa kwenye nchi ambazo ni rafiki wa Tanzania. Kwamba wanafunzi kwenye chuo hicho wanafundishwa na kuivushwa namna ya kufanya upelelezi na kukusanya ushahidi bila kumuumiza au kumlazimisha mtuhumiwa. Lakini pia idara hii inakuwa na askari ambao wanafundishwa namna ya kudhibiti vurugu bila kuua au kuvunja viungo watuhumiwa kama wanavyofanya hawa vibaka wenu. Tukianzisha idara hii itasaidia sana kwenye nyakati hizi ambazo technology imekua na watu hawaibi tena kwa bunduki na badala yake wanaiba kwa kutumia akili na technology. Huu ushauri kwa undani zaidi upo katika kitabu changu lakini pia ulishawahi kuchapishwa kwenye baadhi ya magazeti. Mdude Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.

Mdude Nyagali

39,775 Aufrufe • vor 1 Jahr