millardayo's banner
millardayo's profile picture

millardayo

@millardayo3,138,054 subscribers

Award winning TV/Radio Personality | Hosting Amplifaya on CloudsFM |Journalist from Tanzania covering East Africa and beyond | Bookings [email protected]

Shorts

Mtoto mdogo ameibua hisia na kuvutia maelfu ya Watu baada ya kuonyesha ujasiri wa kipekee kwa kumkimbilia Papa Leo XIV mara baada ya ibada ya Misa nchini Cameroon. Katika tukio hilo, mtoto huyo ameonekana kuvuka eneo la usalama bila woga na kumfikia Papa, hatua iliyowashangaza walinzi pamoja na waumini waliokuwepo. Badala ya taharuki, Papa alionekana kumkaribisha kwa utulivu na upendo, akionesha ishara ya ukarimu na kujali, jambo lililowagusa wengi waliokuwa wakishuhudia tukio hilo. Wengi mitandaoni wamesifu ujasiri wa mtoto huyo, wakieleza kuwa kitendo chake kinaonyesha imani ya dhati na moyo wa kumwamini kiongozi huyo wa dini, huku wengine wakivutiwa na namna Papa alivyolipokea tukio hilo kwa upole na busara. Tukio hilo sasa limegeuka kuwa gumzo, likitafsiriwa kama picha ya uhusiano wa karibu kati ya viongozi wa dini na waumini wao, hasa watoto. #MillardAyoUPDATES

Mtoto mdogo ameibua hisia na kuvutia maelfu ya Watu baada ya kuonyesha ujasiri wa kipekee kwa kumkimbilia Papa Leo XIV mara baada ya ibada ya Misa nchini Cameroon. Katika tukio hilo, mtoto huyo ameonekana kuvuka eneo la usalama bila woga na kumfikia Papa, hatua iliyowashangaza walinzi pamoja na waumini waliokuwepo. Badala ya taharuki, Papa alionekana kumkaribisha kwa utulivu na upendo, akionesha ishara ya ukarimu na kujali, jambo lililowagusa wengi waliokuwa wakishuhudia tukio hilo. Wengi mitandaoni wamesifu ujasiri wa mtoto huyo, wakieleza kuwa kitendo chake kinaonyesha imani ya dhati na moyo wa kumwamini kiongozi huyo wa dini, huku wengine wakivutiwa na namna Papa alivyolipokea tukio hilo kwa upole na busara. Tukio hilo sasa limegeuka kuwa gumzo, likitafsiriwa kama picha ya uhusiano wa karibu kati ya viongozi wa dini na waumini wao, hasa watoto. #MillardAyoUPDATES

24,411 görüntüleme

Refa wa Somalia, Omar Abdulkadir Artan amerejea Nchini kwao baada ya kuzuiwa kuingia Marekani ambapo alitarajiwa kuwa miongoni mwa waamuzi wa Kombe la Dunia 2026. Artan alikuwa ameandika historia kwa kuchaguliwa na FIFA kuwa mwamuzi wa kwanza kutoka Somalia kushiriki katika fainali za Kombe la Dunia. Hata hivyo, alizuiwa kuingia Marekani katika Uwanja wa Ndege wa Miami licha ya kuwa na visa halali ya kusafiria. FIFA baadaye ilithibitisha kuwa hatashiriki mashindano hayo kutokana na kushindwa kuingia Nchini humo. Akizungumza leo Juni 10, 2026 baada ya kupokelewa Nchini kwao Somalia, Artan aliwashukuru FIFA, CAF na Wananchi wa Somalia kwa sapoti waliyoendelea kumpatia licha ya kukosa nafasi hiyo muhimu katika maisha yake ya uamuzi. Kwa sasa, taarifa zinadai kuwa kuna Mfanyabiashara mmoja wa Somalia amempa Omar Artan dola 100,000 (shilingi milioni 262) kama pole lakini bado hazijathibitishwa rasmi na Vyanzo Vikuu vya Habari. #MillardAyoAUPDATES

Refa wa Somalia, Omar Abdulkadir Artan amerejea Nchini kwao baada ya kuzuiwa kuingia Marekani ambapo alitarajiwa kuwa miongoni mwa waamuzi wa Kombe la Dunia 2026. Artan alikuwa ameandika historia kwa kuchaguliwa na FIFA kuwa mwamuzi wa kwanza kutoka Somalia kushiriki katika fainali za Kombe la Dunia. Hata hivyo, alizuiwa kuingia Marekani katika Uwanja wa Ndege wa Miami licha ya kuwa na visa halali ya kusafiria. FIFA baadaye ilithibitisha kuwa hatashiriki mashindano hayo kutokana na kushindwa kuingia Nchini humo. Akizungumza leo Juni 10, 2026 baada ya kupokelewa Nchini kwao Somalia, Artan aliwashukuru FIFA, CAF na Wananchi wa Somalia kwa sapoti waliyoendelea kumpatia licha ya kukosa nafasi hiyo muhimu katika maisha yake ya uamuzi. Kwa sasa, taarifa zinadai kuwa kuna Mfanyabiashara mmoja wa Somalia amempa Omar Artan dola 100,000 (shilingi milioni 262) kama pole lakini bado hazijathibitishwa rasmi na Vyanzo Vikuu vya Habari. #MillardAyoAUPDATES

10,597 görüntüleme

Usione vyaelea, ujue vimeundwa….. 😀 leo nina elfu hamsinihamsini 5 za kuwapa Watu watano hapa X wataotisha na misemo ya kiswahili inayoendana na hii video ya maji yangu pendwa ya AFYA 🫶🫶🏿 Afya Pure Drinking Water

Usione vyaelea, ujue vimeundwa….. 😀 leo nina elfu hamsinihamsini 5 za kuwapa Watu watano hapa X wataotisha na misemo ya kiswahili inayoendana na hii video ya maji yangu pendwa ya AFYA 🫶🫶🏿 Afya Pure Drinking Water

114,707 görüntüleme

Ni mwendo wa kutunga sentensi tu wiki hii……. hapa nina elfu ishiriniishirini kwa Watu 10 wataopatia kutunga sentensi kwa kuunganisha hefuri hizi tatu za A.B.F !!! sentensi yako isikose maneno haya mawili ya AFIYA BERRIES!! ……….twende kazi

Ni mwendo wa kutunga sentensi tu wiki hii……. hapa nina elfu ishiriniishirini kwa Watu 10 wataopatia kutunga sentensi kwa kuunganisha hefuri hizi tatu za A.B.F !!! sentensi yako isikose maneno haya mawili ya AFIYA BERRIES!! ……….twende kazi

85,229 görüntüleme

Jioni ya jana imefanyika hafla fupi ya chakula cha jioni katika Jiji la Johannesburg, hafla hiyo maalum iliandaliwa na Rais wa CAF Patrice Motsepe akimkaribisha Rais wa FIFA Gianni Infantino nchini Afrika Kusini. Viongozi wakubwa wa mpira Duniani wamehudhuria hafla hiyo akiwemo Rais wa Klabu ya Yanga Hersi Ally Said ambapo amekutana na Rais wa FIFA Gianni Infantino akiwa na Mwenyeji wake Rais wa CAF Patrice Motsepe na miongoni mwa mambo ambayo Rais wa FIFA Gianni Infantino aliyauliza Hersi ni matokeo ya ‘Derby’ ya Kariakoo iliyochezwa November 5,2023 ambapo Hersi alimjibu kuwa waliipiga Simba bao tano. #MillardAyoUPDATES

Jioni ya jana imefanyika hafla fupi ya chakula cha jioni katika Jiji la Johannesburg, hafla hiyo maalum iliandaliwa na Rais wa CAF Patrice Motsepe akimkaribisha Rais wa FIFA Gianni Infantino nchini Afrika Kusini. Viongozi wakubwa wa mpira Duniani wamehudhuria hafla hiyo akiwemo Rais wa Klabu ya Yanga Hersi Ally Said ambapo amekutana na Rais wa FIFA Gianni Infantino akiwa na Mwenyeji wake Rais wa CAF Patrice Motsepe na miongoni mwa mambo ambayo Rais wa FIFA Gianni Infantino aliyauliza Hersi ni matokeo ya ‘Derby’ ya Kariakoo iliyochezwa November 5,2023 ambapo Hersi alimjibu kuwa waliipiga Simba bao tano. #MillardAyoUPDATES

93,927 görüntüleme

VIDEO: Mastaa wa Bongofleva Diamond Platnumz na Harmonize jioni ya leo wamekutana Ikulu Jijini Dar es salaam na kusalimiana kwa kupeana mikono wakati wa futari iliyoandaliwa na Rais Samia na kuwaalika Watu mbalimbali wakiwemo Wasanii. Harmonize alionekana kumfuata na kumsalimia Diamond aliyekua ameka pembeni ya Meneja Sallam ambapo katika sehemu ya maongezi yao, Harmonize alisikika akimwambia Diamond ‘nitakupigia kesho, pokea basi’. Harmonize alisainiwa na Lebo ya WCB zaidi ya miaka tisa iliyopita lakini aliondoka kwenye lebo hiyo miaka zaidi ya minne iliyopita na toka hapo uhusiano wa wawili hao ulivunjika. #MillardAyoUPDATES

VIDEO: Mastaa wa Bongofleva Diamond Platnumz na Harmonize jioni ya leo wamekutana Ikulu Jijini Dar es salaam na kusalimiana kwa kupeana mikono wakati wa futari iliyoandaliwa na Rais Samia na kuwaalika Watu mbalimbali wakiwemo Wasanii. Harmonize alionekana kumfuata na kumsalimia Diamond aliyekua ameka pembeni ya Meneja Sallam ambapo katika sehemu ya maongezi yao, Harmonize alisikika akimwambia Diamond ‘nitakupigia kesho, pokea basi’. Harmonize alisainiwa na Lebo ya WCB zaidi ya miaka tisa iliyopita lakini aliondoka kwenye lebo hiyo miaka zaidi ya minne iliyopita na toka hapo uhusiano wa wawili hao ulivunjika. #MillardAyoUPDATES

70,774 görüntüleme

Videos

millardayo's profile picture

Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Kigoma imeanza kusikiliza kesi ya uchaguzi inayopinga ushindi wa Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia CCM, Clayton Chipando maarufu Baba Levo. Kesi hiyo imefunguliwa na Wananchi wanne wa Jimbo la Kigoma Mjini, Johary Kabourou, Loum Mwitu, Pendo Kombolela na Luma Akilimali ambao pia wameishtaki Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) wakipinga matokeo ya uchaguzi huo. Baba Levo alitangazwa mshindi wa kiti cha ubunge cha Jimbo la Kigoma Mjini katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 baada ya kumshinda mgombea wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe. Katika kesi ya uchaguzi namba 28949 ya mwaka 2025, wadai hao wanaojitambulisha kuwa Wapiga Kura wa Jimbo la Kigoma Mjini, wanadai kuwa uchaguzi huo ulikuwa na kasoro mbalimbali ambazo kwa mujibu wao, ziliathiri uhalali wa matokeo yaliyotangazwa. Shauri hilo linasikilizwa na Jaji Victoria Nongwa ambapo awali lilipangwa kuanza Juni 18, 2026, lakini likaahirishwa baada ya Walalamikaji kushindwa kuwasilisha kwa wakati maelezo ya maandishi ya mashahidi wanaotarajiwa kutoa ushahidi mahakamani, kama zinavyoelekezwa na Kanuni za Mashauri ya Uchaguzi wa Wabunge za Mwaka 2025. Leo, pande zote zimeanza kuwasilisha hoja zao mbele ya Mahakama huku shauri hilo likiendelea kufuatiliwa kwa karibu na Wananchi wa Kigoma na Wadau wa Siasa kutokana na umuhimu wake katika kuamua uhalali wa matokeo ya uchaguzi wa Jimbo la Kigoma Mjini. #MillardAyoUPDATES

millardayo

42,453 görüntüleme • 8 gün önce

millardayo's profile picture

Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) limefuta matokeo ya Watahiniwa 58 baada ya kubainika kufanya udanganyifu katika mitihani iliyofanyika Mei 2026 ikiwemo kutumia ChatGPT ambayo ni programu ya Akili Bandia (AI). Akizungumza leo Julai 6, 2026 Jijini Dar es salaam, Katibu Mtendaji wa NECTA, Prof. Said Mohamed amesema katika udanganyifu uliofanyika wapo walioingia na notisi, waliokamatwa na simu kwa kutumia ChatGPT na kusaidiana majibu. Kwa mujibu wa NECTA, Watahiniwa waliofutiwa matokeo ni 44 wa Mtihani wa Kidato cha Sita (36 wa shule na 8 wa kujitegemea) pamoja na Watahiniwa 14 wa Mtihani wa Stashahada ya Ualimu wa Elimu ya Msingi (DPEE). Prof. Mohammed amesema hatua hiyo imechukuliwa kwa mujibu wa Kifungu cha 5(2)(i) na (j) cha Sheria ya Baraza la Mitihani, Sura ya 107, kikisomwa pamoja na Kifungu cha 30(2)(b) cha Kanuni za Mitihani za Mwaka 2016. Aidha, amesema imekifungia Kituo cha Mitihani cha Excellency Open School (P5584) kilichopo Mkoani Manyara kuendelea kutumika kama Kituo cha Mitihani ya Taifa, baada ya kubainika kukiuka miongozo ya uendeshaji wa mitihani ambapo Kituo hicho kitabaki kufungwa hadi Baraza litakapojiridhisha kuwa kinafaa kwa uendeshaji wa Mitihani ya Taifa. Katika taarifa hiyo, NECTA pia imezipongeza Kamati za Uendeshaji Mitihani za Mikoa na Halmashauri, Wakuu wa Shule, Wasimamizi, Wasahihishaji wa mitihani pamoja na Watahiniwa wote waliozingatia taratibu za mitihani. Baraza limeeleza kuwa matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Sita (ACSEE) na mitihani ya Ualimu iliyofanyika Mei 2026 yanapatikana kupitia tovuti yake rasmi. #MillardAyoUPDATES

millardayo

22,834 görüntüleme • 8 gün önce