
Mohammed Dewji MO
@moodewji • 2,302,341 subscribers
Pan-African Entrepreneur, President @MeTL_Group & @SimbaSCTanzania, Philanthropist @DewjiFoundation, Georgetown Alumni #Hoya
Shorts
Videos

Umekuwa wakati mzuri kupata muda wa kuzungumza na kuwapa hamasa wachezaji pamoja na benchi la ufundi. Kama klabu, tunapaswa kubaki pamoja, kuwa na utulivu, na kuendelea kupambana hadi mwisho. Kwenye mpira, lolote linawezekana. Never retreat. Never surrender. 🦁 #Simba #NguvuMoja
Mohammed Dewji MO11,792 views • 18 days ago

Hapa unadhani ninafikiria nini? 🤔 Jibu bora zaidi litapokea zawadi 👇🏽👇🏽
Mohammed Dewji MO245,121 views • 1 year ago

Kujikwa si kuanguka, bali ni kwenda mbele. 🦁Tupo Pamoja!
Mohammed Dewji MO199,539 views • 2 years ago

#Discipline in one area of life spills over into all others. My daily fitness routine is more than just staying in shape—it sharpens my focus, builds resilience, and strengthens my mindset. 🏓💪🏽 Whether in business, sports, or life, consistency is the real game-changer. #Paddle keeps me moving and thinking fast—big thanks to my coach Conor Silkman 🙏🏽 #Fitness #Mo
Mohammed Dewji MO98,035 views • 1 year ago
0:49
Sensitive content
This media may contain sensitive content.

Leo ni siku ya kipekee katika historia ya klabu yetu - nusu fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika, hapa nyumbani kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar. Tumefika mbali, lakini safari bado inaendelea. Mbele yetu kuna nafasi ya kuingia fainali na kuiweka Simba kwenye ramani ya soka la Afrika kwa kiwango cha juu kabisa. Nimewahi kutembelea Stellenbosch na ninawaheshimu sana kama wapinzani. Lakini ninajua nguvu ya Simba. Juzi nilizungumza na wachezaji wetu kupitia Zoom, niliwaambia wanayo nafasi ya kuandika historia mpya. Niliwaona wakiwa na ari, umoja, na kiu ya mafanikio. Hii ni timu yenye moyo wa ushindi. Safari haijakuwa rahisi. Tulianza msimu huu tukiwa na uso mpya - wachezaji wapya, kocha mpya, benchi la ufundi jipya, na mwelekeo mpya. Lakini tumekabiliana na kila changamoto na tumevuka. Leo ni siku ya kupambana tena. Chezeni kwa moyo, kwa ujasiri, na kwa kujiamini. Hii ni nafasi ya kuweka alama isiyofutika katika historia ya klabu yetu. 📌HATUISHII HAPA #Simba #Nguvumoja —President Simba SC Mohammed Dewji
Mohammed Dewji MO41,207 views • 1 year ago

Tanzania is a nation of extraordinary beauty and opportunity. From world-class tourism to strategic minerals like graphite for the EV future, our country remains one of Africa’s most promising markets. Above all, our strength is our people — resilient, hopeful, and united. May we continue working together to build the future we deserve. Happy 64th Independence Day. 🇹🇿 #Tanzania is worth believing in.
Mohammed Dewji MO21,016 views • 5 months ago

Question for innovators: If you received funding today from a Startup Fund to build with AI, what problem would you solve first in Tanzania or Africa? // Swali kwa wabunifu: Kama ungepata ufadhili leo kutoka Mfuko wa Ubunifu, ni tatizo gani ungelitatua kwanza Tanzania au Afrika kwa kutumia AI? #VijanaNaTeknolojia #StartUpFund #OneMinutewithMo #MoAfrica #AfricanInnovation
Mohammed Dewji MO18,996 views • 5 months ago

Mipango yetu imeanza kuchukua hatua! Maendeleo ya uwanja wa mazoezi Bunju na uanzishwaji wa Mo Simba Arena ni hatua kubwa mbele kwa Simba. Tunajenga mazingira bora kwa wachezaji wetu na kitovu cha ushirikiano wa kijamii. Huu ni msingi wa mabingwa wa leo na kesho! #nguvumoja🦁
Mohammed Dewji MO49,799 views • 1 year ago

Kwa nini Waafrika hatuzalishi chakula chetu wenyewe? Kuna 30% hadi 40% ya ardhi ya kilimo, na idadi kubwa ya vijana. Maono yangu ni kupunguza uagizaji wa chakula kutoka nje kwa 50% na kupata mbadala wa angalau 25% ya bidhaa kama mafuta, nafaka, mahindi na ngano kutoka nje.
Mohammed Dewji MO45,754 views • 2 years ago

Wanasimba, tukutane kwa Mkapa Ijumaa!🦁🦁#AFL #WenyeNchi #NguvuMoja
Mohammed Dewji MO48,620 views • 2 years ago

Wanasimba wenzangu, Kesho ni siku muhimu katika historia ya klabu yetu. Tumefika hatua kubwa—robo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika—lakini safari bado haijaisha. Mbele yetu kuna nafasi ya kuandika historia mpya. Kwa wachezaji wetu mashujaa, mmefika hapa kwa bidii, nidhamu, na moyo wa kujituma. Sasa ni wakati wa kupambana zaidi, kwa umoja, ari, na maono makubwa. Mkumbuke, hamchezi kwa ajili yenu pekee, bali kwa mamilioni ya mashabiki wanaowaamini, kwa heshima ya jezi mnayovaa, na kwa hadhi ya Simba Sports Club. Msimu huu haukuwa rahisi—tulianza na kikosi kipya, benchi jipya la ufundi, na mwalimu mpya, Kocha Fadlu Davids. Pamoja, mmeunda timu imara yenye mshikamano na ari ya ushindi. Kufika hapa ni ushahidi wa juhudi zenu na kujitolea kwenu. Tuna imani nanyi, na tunasimama nanyi katika safari hii. Huu ndio wakati wa Simba kupiga hatua nyingine mbele. Pambaneni kwa moyo, chezeni kwa kujiamini, na tuweke rekodi mpya kwa klabu yetu! Mungu atutangulie. #Simba #NguvuMoja! — Mohammed Dewji Rais, Simba SC
Mohammed Dewji MO27,091 views • 1 year ago