Loading video...

Video Failed to Load

Go Home

Kijana Julieth Jonas anayeshiriki katika programu ya Building a Better Tomorrow (BBT) amesema Vijana wanaweza kuanza shughuli za kilimo kwa mtaji wa Sh100,000 akitaja kilimo cha mbogamboga na alizeti kuwa miongoni mwa fursa zenye uwezo wa kuwaletea kipato hasa kwa Vijana waliopo Dodoma Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea...

50,790 views • 26 days ago •via X (Twitter)

0 Comments

No comments available

Comments from the original post will appear here

Related Videos

Serikali imetoa mikopo yenye thamani ya Shilingi bilioni 76 kwa Vijana na Wanawake 2,366, ikiwa ni sehemu ya kuwawezesha kupata mitaji na kujenga shughuli za kiuchumi, Waziri wa Kilimo, Daniel Chongolo, amesema hayo wakati wa maadhimisho ya kilele cha Nanenane 2026 yanayofanyika Jijini Dodoma. Waziri Chongolo amesema mikopo hiyo imetolewa kupitia Benki ya Ushirika, kwa kushirikiana na Mfuko wa Uthamini wa Pembejeo za Kilimo (AGDF), huku ikiwa na riba isiyozidi asilimia tisa hatua ambayo inalenga kuwawezesha Vijana na Wanawake kupata mitaji yenye masharti nafuu. Aidha, amesema Serikali inaendelea kushirikiana na taasisi za fedha Nchini kutoa mikopo kwa Vijana Wajasiriamali na Wanawake wanaojihusisha na mnyororo wa thamani wa kilimo, biashara ya kilimo, mifugo na uvuvi. Kwa mujibu wa Waziri Chongolo, mpango huo unatekelezwa pia kupitia mradi wa BBT (Jenga Kesho Iliyo Bora), unaolenga kuongeza fursa za Vijana kupata huduma za kifedha na kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji. Katika hatua nyingine, Waziri Chongolo amesema Serikali imepitisha kanuni zinazowataka wachakataji na waagizaji wa mafuta ya kula kutoka nje ya Nchi kuwa na mashamba ya kuzalisha mbegu za mafuta, ikiwemo alizeti na chikichi, pamoja na kuwa na viwanda vya kuchakata mafuta hayo. Amesema waagizaji wataruhusiwa kuleta mafuta kutoka nje pale tu ambapo uzalishaji wa ndani hautatosheleza mahitaji ya soko, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji wa ndani, kupunguza utegemezi wa bidhaa kutoka nje na kuwaongezea wakulima soko la mazao ya mbegu za mafuta. #MillardAyoUPDATES

millardayo

22,848 views • 22 days ago

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda amesema Rais Samia Suluhu Hassan anakwenda kuufungua mkoa wa Arusha kwa ujenzi wa barabara ambazo zitasaidia kuimarisha shughuli za kiuchumi zikiwemo za kilimo na utalii katika Mkoa huo. Makonda ameeleza hayo leo Juni 8, wakati akizungumza na Wananchi katika eneo la Usa River Wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha, wakati Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla akihitimisha ziara yake mkoani humo akielekea Kilimanjaro. Akizungumza Makonda Amesema changamoto iliyopo kwa kiasi kikubwa kwa Wananchi wa Arumeru ni Barabara na kuongeza kuwa Serikali katika kulitambua hilo imeweka mikakati kutatua changamoto hiyo na kuainisha Barabara zinazotarajiwa kujengwa Arumeru na Mkoa wa Arusha kwa ujumla. Makonda amesema Mkoa wao ni wa uchumi wa utalii na kilimo cha mazao ambayo ni chachu katika sekta ya utalii. Makonda amesema katika Barabara ya kutoka Tengeru hadi Usa River tayari Mkandarasi ameshapatikani kwa ajili ya ujenzi wa Barabara ya njia nne kwa takribani kilometa 11.3. Pia amesema walikaa katika kikao cha bodi ya Barabara ya mkoa katika kutafuta utatuzi wa changamoto wa kimkakati na si kwa kupiga kelele alimuomba Waziri wa Ujenzi kufika akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara, Waziri wa fedha, Mkurugenzi Mkuu wa Tanroad na mtubwa ukarabati. “Matokeo ta mkutano huo ukazalisha kuanzia pale USA River tunakwenda kujenga njia nne urefu wa Kilometa 28 mpaka Uwanaj wa Ndege wa Kilimanjaro na hivi ninavyoongea mheshimiwa mwenezi atayari Rais ameshatuma timu na usanifu wa ujenzi umekamilia,” amesema Makonda. Ameongeza kukamilika kwa barabara hiyo kutasaidia watu watatoka uwanja wa ndege wa KIA na kufika moja kwa moja Arusha, pia amesema kuna barabara ya kutoka Tengeru hadi Mirerani yenye urefu wa kilometa 28 Pia kutoka Mirerani hadi Kilimajaro imeingizwa kwenye mpango wa ilani ya CCM usanifu wake umekamilika na kuingizwa kwenye bajeti ya mwaka 2025/2026 na inakwenda kujengwa kwa kiwango cha lami. #MillardAyoUPDATES

millardayo

25,326 views • 1 year ago

Rais Samia Suluhu shikamoo. Umeibua mjadala mzuri na tutajadili pamoja. Nashauri wasaidizi wako wakufikishie sehemu ya maoni yangu katika mjadala huu ulioibua Ughaibuni. Kwa kutumia tafsiri yako ya umaskini, hatutakuwa na mjadala sahihi. Tafsiri ya utajiri haiwezi kuwa tu na uwezo wa kupata chakula na matunda. Hapana. Hata kazi ta Umoja wa Mataifa katika Kutokomeza Umasikini inahusishwa na Malengo ya Maendeleo Endelevu. Wameyataja na kuyainisha malengo 17. Baadhi ya malengo ni; 1. Kutokomeza Umaskini 2. Kukomesha Njaa 3. Afya Njema na ustawi 4. Elimu bora 5. Usawa na jinsia 6. Maji Salama na Usafi. Lazima tutoe tafsiri ya umaskini kwa kutumia tafsiri za viwango vya Umskini vilivyowekwa na Umoja wa Mataifa. Na hapo tutakuwa na mjadala mzuri. Mwaka 1998, Umoja wa Mataifa (UN) ulipitisha Taarifa kuhusu Umaskini (statement on poverty) ilitiwa saini na wakuu wa mashirika yote ya UN. Kimsingi, umaskini ni kunyimwa chaguo na fursa, ukiukaji wa utu wa binadamu . Inamaanisha ukosefu wa msingi. uwezo wa kushiriki kikamilifu katika jamii. Kutokuwa na chakula kulisha familia, kutokuwa na shule, zahanati ya kwenda, kutokuwa na ardhi ya kulima chakula cha mtu au kazi ili kujipatia riziki, Uwezekano wa kukabiliwa na vurugu, na mara nyingi inamaanisha kuishi kwenye mazingira ya pembezoni au tete, bila kupata maji safi na salama au vyoo. Sasa tunaweza kujadili kwa kuzingatia tafsiri hiyo ya Umoja wa mataifa (UN) kuhusu Umaskini ambayo ilitiwa saini na wakuu wa mashirika yote ya UN. Tanzaniani inazo rasilimali nyingi lakini wananchi wake ni maskini wa kutupwa. Rasilimali walizonazo haziwanufaishi kabisa na zinatumiwa hovyo. Pamoja na mikakati mingi ya kutokomeza umaskini, bado umaskini umeendelea kuwa adui wa Taifa. Viongozi wengi kama siyo wote siyo waaminifu. Hata Wanaokiuka maadili na ukosefu wa uaminifu hawachukuliwi hatua za kisheria. Wanahamishwa kutoka eneo moja la kazi na kwenda eneo lingine. Kuna ukosefu mkubwa sana wa maadili kwa watumishi na viongozi wa umma. Wamejitajirisha kupitia mali za umma. Wanao utajiri wa kutisha. Wamejitajirisha kupitia nafasi zao katika utumishiwa huo wa umma, vyanzo vyao havieleweki. Watanzani wengi wanamiliki umasikini wa kutisha sana. Tanzania ina jumla la eneo ukubwa wa 947,303 km² (30th Duniani). Eneo lenye maji 6.4%. 93.6% ni eneo la nchi kavu. 45% ya ardhi yote inafaa kwa kilimo. Eneo ambalo limetumika kwa ajili ya kilimo halijafika hata 30%. Kwanini kama ncji sasa tusiwekeze katika kilimo chenye tija na tukatafute kodi nyingi? Ardhi ya Kilimo (% ya eneo la ardhi) Tanzania ilikuwa 44.62% kufikia 2020, kulingana na ukusanyaji wa viashiria vya maendeleo vya Benki ya Dunia, Viashiria vilivyokusanywa kutoka vyanzo mbalimbali ambavyo vinatambulika na Benki ya Dunia (World Bank) hadi kufikia kipindi cha kuanzia Januari 2023 Kufikia ¼ ya nne ya mwaka 2021 (Q4 2021), shughuli za kilimo zilichangia karibu 30% ya Pato la Taifa la Tanzania (GDP). Ni karibu nusu ya pato lote la Taifa. Mwaka 2020, ilifikia 26.9%. Kilimo ni moja ya sekta kuu za kiuchumi Tanzania. Tangu 2012, mchango wake katika uchumi wa nchi umebaki juu ya 25%. Vijijini 78% ya Watanzania wanajihusisha na Kilimo. Wananchi vijijini hawafanyi uzalishaji. Hii ni hatari sana, ni dalili kuwa ufukara wa watu wetu unazidi. Zaidi ya nchi 80 Duniani huzalisha ngano duniani kote, uzalishaji mkubwa wa ngano duniani unatoka katika nchi chache tu ambazo haziwezi kuzidi nchi 10. Kulingana na takwimu za Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO). Tanzania haipo katika orodha hiyo. Watawala wameshindwa kabisa kufikiri. Tanzania inanunua zaidi ya tani 1,000,000 za ngano kutoka nje. Hivyo kwa mwaka Tanzania inatumia zaidi ya Sh1.3 trilioni kuagiza chakula kutoka nje ya nchi. Sekta ya kilimo ni msingi wa Uchumi Tanzania. 65.5% ya watanzania wameajiriwa kwenye kilimo au wanategemea kilimo kwa kipato chao cha kila siku,. 100% ya chakula inategemewa kutoka sekta ya kilimo. Kilimo kinachangia 29.1% ya pato la taifa (GDP), karibia ⅓ ya thamani ya shughuli za Uchumi. Nimeshauri sana, wezesheni vijana eneo la fedha na masoko, vijana wafanye uzalishaji. Fungamanisha sekta ya kilimo na viwanda ili kutegemeana kisekta Wekezeni katika kilimo chenye tija, tumieni kilimo kama fursa ya kutuvusha kufika mnapotaka, kodi nyingi hazitotufikisha tunapohitaji kufika kama taifa. Mtatuumiza tu. Fursa ya soko ipo sana Duniani. Hali ya mahitaji ya chakula Duniani mwaka 2020 takribani watu milioni 811 walikuwa hawana lishe bora China ni mzalishaji mkubwa zaidi wa ngano Duniani, imetoa zaidi ya tani bilioni 2.4 za ngano katika miaka 20 iliyopita, na hii ni karibu 17% ya jumla ya uzalishaji. Nchi ya pili Duniani kwa uzalishaji wa ngano ni India. Katika miongo miwili, India imetoa 12.5% ​​ya ngano yote ya Duniani. Hawa ni wauzaji wakubwa wa ngano. Kama ilivyo kwa China, India pia inahifadhi ngano yake nyingi ndani kwa mahitaji makubwa ya chakula ndani ya nchi zao. Nchi ya India ina wakazi 1.4 bilioni. Katika orodha hii, Ukraine anashika nafasi ya 10, katika miongo 2 iliyopita wamezalisha tani milioni 433 za ngano, karibu 3.1% ya jumla ya uzalishaji Russia, nchi ya tatu Duniani kwa uzalishaji wa ngano, ni muuzaji mkubwa wa ngano kimataifa. Pia, Russia kama zilivyo China na India wanahifadhi ngano yao. Russia ilisafirisha ngano yenye thamani ya zaidi ya dola bilioni 7.3 kwa 2021, ikichukua takribani 13.1% ya jumla ya mauzo ya ngano mwaka huo Duniani. Kulingana na takwimu za Idara ya Kilimo ya Marekani (US Department of Agriculture), Ukraine ilikuwa nchi ya 7 kwa uzalishaji wa ngano Duniani kufikia 2021. Ukraine 2021/22 ikizalisha tani milioni 33. Australia, Marekani, Russia, India na China ndizo zilizozalisha zaidi. Ukraine ni ndogo sana kwa Tanzania. Takribani 80% ya uzalishaji wa kilimo Tanzania unatokana na wakulima wadogo, wanategemea kilimo cha mikono na uzalishaji kutegemea mvua. Kilimo cha mikono na uzalishaji wa kutegemea mvua huwafanya kuwa katika hatari ya majanga ya mabadiliko ya hali ya hewa. Wizara ya kilimo ipo? Kilimo, ni tegemeo kuu la maisha kwa takribani 70% ya kaya za Tanzania, kilimo kinakuwa taratibu sana. Sekta ya kilimo, inaundwa na wakulima wadogo. Sekta ya kilimo haijanufaika na kasi sawa na sekta nyingine na inahitaji uwekezaji na kisasa. Vijana wanachangia 30% ya nguvu kazi, hasa katika kilimo. Umaskini umeenea vijijini, makazi ya zaidi ya 70% ya watu ambao ni maskini. Ukweli, ukuaji wa uchumi umeshuka hadi kwa watu maskini wa Tanzania. 70% ya Watanzania wanaendelea kuishi chini ya $2.00 kwa siku. Tanzania inayo 45% ya ardhi ambayo inafaa kwa kilimo na 30% ya matumizi hayajafikiwa. Ni kwa sababu hii, pamoja na uchumi kukua, 7% kwa mwaka, lakini bado wananchi wetu walio wengi wanaishi kwenye dimbwi la ufukara. Maana ukuaji huo wa Uchumi hauhusishi kilimo ambacho kimetoa ajira kwa watanzania karibu 70%, hauhusishi zaidi ya robo 3 ya Watanzania. Hatari. Hapa unapiga ramli kutafuta mchawi? Tunapaswa kujiuliza wenzetu wamefanya uchawi gani kuwa na maendeleo? Mchawi ni SERIKALI ya CCM. Kwa mujibu wa wataalamu wa Uchumi, ili kupunguza umasikini Tanzania, sekta ya kilimo inapaswa kukua kwa zaidi ya 8% angalau kwa miaka 3 mfululizo, Na wataalam hao wa uchumi kwa tafiti wanasisitiza kwamba ukuaji huo wa sekta uendelee kukua kwa wastani wa 6% kwa muda miaka 10 mfululizo. Watawala awamu zote na hata waliopo madarakani wameshindwa kutekeleza wajibu wao ipasavyo. Wamechoka. Wapumzishwe. Nitawapa ushauri! Serikali kupitia wizara ya kilimo inawajibika kujenga mnyororo wa thamani. Mnyororo unaojumuisha zaidi na ustahimilivu wa bidhaa za kipaumbele, Serikali yenye kutumia ubongo lazima ihangaike na masuala yanayowahusu wananchi walio wengi, na hapa Tanzania watu hao (walio wengi) ni Wakulima. Hivyo basi, kipimo kikuu cha kuondoa umasikini wa Watanzania ni kuondoa umasikini wa wakulima. Wakulima wa Tanzania wametelekezwa kabisa. Mnyororo ujengwe katika bidhaa zinazosukumwa na upanuzi endelevu wa upatikanaji wa masoko na huduma za kifedha na kuhakikisha sekta binafsi inajitegemea; Serikali kupitia wizara ya kilimo katika utaratibu wa kibajeti kuboresha teknolojia zinazostahimili hali ya hewa zinazoongeza tija katika mazao ya kipaumbele, Mifugo na bidhaa za uvuvi; Tanzania kama nchi nyingine, inakumbwa na athari za mabadiliko ya tabia ya nchi. Serikali iwekeze katika teknolojia ya kilimo. Serikali ihusike katika kuimarisha utawala bora wa ardhi, na kuwezesha uwekezaji wa umma na uwekezaji binafsi katika kilimo. BBT ni failed project. Wananchi wapewe fursa na wawezeshwe mitaji na pembejeo ili wazalishe na serikali iwatafutie masoko ya bidhaa. Wazalishe mazao ya chakulana biashara. Ni wajibu wa Serikali ambao wanaukwepa. Serikali hii naelewa haiwezi kuleta tena tija kwa muda mfupi sana uliobaki. CCM mnahitaji miaka 100 kutekeleza. Matendo ya Serikali yako yanaonyesha tofauti, Serikali haiwajali wanyonge, inapuuza uchumi wa 65.5% ya hao watu ambao unawaita siyo maskini. Ni vigumu kuondoa umasikini mkiendelea kuwadharau wakulima. Kilimo ni sekta ya msingi, ni uti wa mgongo wa uchumi wa Taifa, ni sekta nyeti. Lakini itafaa nini ikiwa umaskini wa watanzania ni fursa ya kisiasa kwa watawala wa CCM nyakati zote? Wanautumia umaskini kama fimbo ya kuwachapia. Suluhisho ni moja tu. Ni kubadili mfumo mzima wa Serikali na kuweka kizazi kitakacho-chukia rushwa, wizi, uzembe na matumizi mabaya ya madaraka. MMM, Martin Maranja Masese, Mtikila.

Martin Maranja Masese

38,634 views • 1 year ago