Sensitive content

This media may contain sensitive content.

Video wird geladen...

Video konnte nicht geladen werden

Zur Startseite

Msikilizeni Kwa Umakini PADRI KITIMA🔥🔥

70,317 Aufrufe • vor 1 Jahr •via X (Twitter)

11 Kommentare

Profilbild von UNJUNICIAN💊💉
UNJUNICIAN💊💉vor 1 Jahr

Sasa mtu kama huyu aliyekuwa ana hubiri haki anapata matatizo alafu anatokea mtu mmoja tu na tumbo lake kubwa lililo jaa mafuta anamdhihaki huyu mtu.

Profilbild von 公式:ちぃたん☆広島
公式:ちぃたん☆広島vor 2 Jahren

Experiment how long Chiitan can endure if roll with a crane.

Profilbild von ABDULBASIR MUHAMMAD BENETO☝️
ABDULBASIR MUHAMMAD BENETO☝️vor 1 Jahr

Sasa yanatoka madini tuu💪 Kwa heshima mungu amjalie arudi kwenye Hali yake yakawaida amiiini🤲

Profilbild von free sudan 🇸🇩 , palestina 🇵🇸 and ukraine 🇺🇦
free sudan 🇸🇩 , palestina 🇵🇸 and ukraine 🇺🇦vor 1 Jahr

Honestly Mungu amponye baba yetu huyu.

Profilbild von KINGDANIEL
KINGDANIELvor 1 Jahr

Bro ukiwa mkweli nchii hii unagombana na serikali amini

Profilbild von Bravo Laurent
Bravo Laurentvor 1 Jahr

Padri kitima yupo sahihi sana kama akili zako zipo sahihi utamuelewa

Profilbild von Dr. michael.
Dr. michael.vor 1 Jahr

Haya mambo ya watu kupotea ni mjinga tu pekeake ndonaweza kuyapenda

Profilbild von Elias Vicent
Elias Vicentvor 1 Jahr

Watu kupotea hakujaanza 2015 sema tu ni kwamba uelewa wa watu juu ya matumizi ya mitandao na usambaaji wa taarifa ulikuja zaidi baada ya kipindi hicho kwa mfano, Ulimboka alitekwa 2012,mwangosi aliuwa 2013 kama sijakosea padre evarist mushi paroko wangu parokia ya kitope aliuawa

Profilbild von Onesmo Leckson
Onesmo Lecksonvor 1 Jahr

🔥

Profilbild von go
govor 1 Jahr

Mark this.. Hilo linakuja Haikwepeki

Profilbild von #PowerTheorist
#PowerTheoristvor 1 Jahr

Magufuli deep state inamuendesha sana Mama. they are everywhere . hata alipo wasimamisha Nape na January ilikua kazi yao. walihakikisha kina Kabudi , Biteko , na wengine wanarudi. weakness sasa wana msumbua kumwaharibia

Ähnliche Videos

VIDEO: Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamshikilia mtu mmoja kwa tuhuma za kuhusika katika shambulio dhidi ya Padri Charles Kitima, Katibu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), aliyejeruhiwa kichwani na kitu butu akiwa katika eneo la maliwato ya kantini ya TEC, Kurasini. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Mei 1, majira ya saa nne na robo, muda mfupi baada ya Padri Kitima kuhitimisha kikao cha viongozi wa dini kilichofanyika tangu saa tatu asubuhi hadi saa moja jioni. "Baada ya kikao, Padri Kitima alielekea kwenye kantini ya baraza na kubaki hapo hadi saa nne na robo usiku, alipokwenda maliwatoni na ndipo alipojeruhiwa kichwani na watu wawili waliotumia kitu butu," imeeleza taarifa ya polisi. Padri Kitima alikimbizwa katika Hospitali ya Aga Khan ambapo anaendelea kupatiwa matibabu na hali yake inaelezwa kuwa inaendelea vizuri. Jeshi la Polisi limeeleza kuwa linamshikilia Rauli Mahabi/ Haraja, mkazi wa Kurasini, kwa mahojiano kuhusiana na tukio hilo na linafanya uchunguzi wa kina wa chanzo cha tukio hili na kuwachukulia hatua kali na za haraka wote waliohusika. Awali baadhi ya mashuhuda na waumini wa Kanisa hilo waliokuwepo kwenye mgahawa mmoja ndani ya Viunga vya TEC, Kurasini walieeleza Jambo TV kuwa Padri Kitima akiwa kwenye mazungumzo na baadhi ya watu, alinyanyuka na kuelekea msalani na ghafla kwa dakika chache walitokea watu waliomshambulia kwa sekunde chache na kisha kuondoka, na baadaye ndipo Padri Kitima alipoonekana akiomba msaada akiwa anavuja damu katika sehemu mbalimbali za mwili wake. Mara baada ya shambulizi hilo, Padri Kitima amepatiwa matibabu ya awali kwenye kituo kidogo cha afya cha TEC kilichopo eneo hilo. Padri Kitima kando ya utumishi wake na nafasi aliyonayo ndani ya Kanisa, amejipatia umaarufu mkubwa nchini Tanzania kwa miaka ya hivi karibuni kwa namna ambavyo amekuwa mkosoaji mkubwa wa mienendo isiyofaa kwenye jamii na akiwa mstari wa mbele katika kuhubiri utawala wa sheria na haki za binadamu pamoja na Demokrasia.

Jambo TV

26,317 Aufrufe • vor 1 Jahr