Загрузка видео...

Не удалось загрузить видео

На главную

“Wanakamati tawanyikeni”

19,899 просмотров • 19 дней назад •via X (Twitter)

Комментарии: 0

Нет доступных комментариев

Здесь появятся комментарии из оригинального поста

Похожие видео

Kuna wakati najiuliza maswali mengi sana sipati majibu. Kweli hawa watangazaji wanayo taaluma ya habari? Kama wanayo ni kweli wanatumia ubongo walionao au kichwa kimetumika kama pambo la kubeba nywele? Pili, kujenga miradi ya maendeleo, huo siyo wajibu wa chama cha siasa. Vyama vya siasa havikusanyi kodi. Huo ni wajibu wa serikali ambayo inakusanya kodi. Mnatakiwa kuikasirikia serikali siyo CHADEMA. Serikali ya Tanzania ikusanye kodi za watanzania tena double taxation, pesa zingetumika kujenga madarasa na barabara zinatumika kununua magari ya anasa kwa viongozi wao; wakuu wa wilaya na mikoa. CHADEMA wahamasishe wananchi wachangie tena gharama za ujezi wa barabara, shule, hospitali, umeme, maji? Mtangazaji wa aina hii anaweza kuwa na ubongo unaofanya kazi? Au ndiyo uhuru wa maoni? Wewe mtangazaji kissa_daniel unaujua wajibu wa serikali kwa raia wake kweli? Serikali ina wajibu wa kukusanya kodi kutoka kwa raia wake. Raia wanao wajibu wa kulipa kodi. Hii ni common principle tu. Baada ya kukusanya kodi, Serikali ina wajibu wa kurudisha pesa ilizokusanya kutoka kwa watanzania kuleta maendeleo na kuhudumia jamii. Huduma za jamii ni sambamba na shule na hospitali. Siyo jukumu la walipa kodi kuchangisha fedha kujenga miradi ya maendeleo. Siyo jukumu la chama cha siasa kisichounda serikali kuleta maendeleo. Hilo ni jukumu la serikali. Hivi vitu hamkusoma kwenye URAIA? Wajibu wa mtanzania ni kulipa kodi. Wajibu wa serikali ni kukusanya kodi na kuleta maendeleo ya jamii. Serikali isiyoleta maendeleo na imekusanya kodi ni MFU. Serikali ya aina hiyo inatakiwa KUKATALIWA. Ulipe kodi, kwa kila bidhaa unayotumia kuna kodi ya ongezeko la thamani (Value Added Tax - VAT) wahuni waitafune, halafu uanze kuhamisha wananchi wachangie miradi ya maendeleo? Hiyo ni akili? Mchango wa jamii fulani kununua chombo cha usafiri kwa mtu wao inakuwa vipi tatizo la jamii? Hilo ni jambo lao binafsi. Hiyo ni kama tu jamii inavyochanga michango kwa ajili ya sherehe mbalimbali. Unachotaka kifanyike ni kama hivi, baada ya kutoa michango ya kufanikisha harusi ya rafiki yetu, wanakamati tuhamasishe waliochanga kwenye harusi ya ndugu yetu wachangie miradi ya maendeleo. Pia, ipo Sheria ya Barabara Mwaka 2007 na Kanuni zake za mwaka 2009, hairuhusu mwananchi wa kawaida kutengeneza barabara. Barabara zipo chini ya usimamizi wa TANROADS na TARURA. Kifungu cha 49(e) ni kosa kuchimba, kuongeza, kuondoa au kubadilisha udongo au sakafu ya hifadhi ya barabara au pembezoni mwa barabara. Faini yake ni TZS milioni 1 au kifungo miaka 3 au vyote kwa pamoja. Taarifa za ukaguzi za CAG zinaoesha wahuni wanavyotafuna fedha zetu. Watangazaji mnatakiwa kutumia muda wenu kujadili masuala hayo na kuiweka serikali kitimoto, fedha zirudishwe serikalini. Nafikiri, mtangazaji ana changamoto ya afya akili. Hawezi kuwa timamu, au waajiri wake hawapo makini, na hawafuatilii maudhui ya mwajiriwa wao. Wanatakiwa kurudishwa kwenye semina za kuwajengea uwezo. Pia, sioni kwanini mnaifanya hii kuwa hoja na agenda yenu. Haina maana na hadhi ya kuwa mjadala katika chombo cha habari. Mchango ni jambo la hiari. Halazimishwi mtu kuchanga pesa yake. UCHAWA TU. Brigedia Mtikila, MMM.

Martin Maranja Masese

52,816 просмотров • 2 лет назад

Klo gda cctv g bkal tau dia nih😰
0:52

Sensitive content

Klo gda cctv g bkal tau dia nih😰

noni

13,648,378 просмотров • 1 год назад