ๆญฃๅœจๅŠ ่ฝฝ่ง†้ข‘...

่ง†้ข‘ๅŠ ่ฝฝๅคฑ่ดฅ

๐‚๐€๐๐“๐€๐ˆ๐ ๐…๐€๐๐“๐€๐’๐“๐ˆ๐‚ ๐’๐’…๐’‚๐’๐’Š ๐’š๐’‚ ๐’๐ˆ๐Œ๐๐€ ๐ƒ๐€๐˜ ๐Ÿ๐ŸŽ๐Ÿ๐Ÿ”. Legend John Bocco atakuwa mmoja wa wageni maalumu katika Simba Day 2026, lakini pia atashiriki mchezo wa kirafiki kama mmoja wa wachezaji wa timu ya menejimenti ya Simba. Vuta picha hapa Okwi, pale Kagere na Bocco. Kesho hiyooo. #SimbaWeek2026 #SimbaDay2026 #NguvuMoja

24,068 ๆฌก่ง‚็œ‹ โ€ข 29 ๅคฉๅ‰ โ€ขvia X (Twitter)

0 ๆก่ฏ„่ฎบ

ๆš‚ๆ— ่ฏ„่ฎบ

ๅŽŸๅง‹ๅธ–ๅญ็š„่ฏ„่ฎบๅฐ†ๆ˜พ็คบๅœจ่ฟ™้‡Œ

็›ธๅ…ณ่ง†้ข‘

VIDEO: Viongozi wa matawi ya Young Africans SC na Wazee wa klabu hiyo mkoani Dodoma wametoa tamko kali wakimtaka Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), TFF TANZANIA Wallace Karia, kuomba radhi hadharani kwa kauli alizozitoa kufuatia kuahirishwa kwa mechi ya watani wa jadi, Simba na Yanga. Wakizungumza na wanahabari Jijini Dodoma leo Machi 18, 2025, viongozi na wazee hao wameeleza kutoridhishwa kwao na maamuzi yaliyofanywa, wakidai kuwa wamepoteza imani na Karia na uongozi wake. Mzee Abdalah Mtosa Ally kutoka Tawi la Changโ€™ombe amesema hakuna sababu ya kurudia mechi hiyo kwani tarehe 8 ilikuwa sahihi kwa mchezo huo kufanyika. "Mimi kama mzee wa Yanga Dodoma, kwa masikitiko makubwa, hatuna imani na Karia kwani tunajua wazi hana mapenzi ya dhati na Yanga. Niwaombe viongozi wa juu kutoruhusu mechi hiyo kufanyika tena. Kama ni faini tuko tayari kulipa, lakini siyo kurudia mechi na Simba," amesema Bernard Mtengwa, mmoja wa wazee wa Yanga. Naye Bodar Awadhi Ahmed, mzee mwingine wa Yanga, amesema kuwa uamuzi wa kuahirisha mechi hiyo umeleta mkanganyiko na sintofahamu kwa mashabiki wa soka, huku wengi wao wakipinga kufanyika upya kwa mchezo huo. Aidha, viongozi hao wamesisitiza kuwa hawana tena imani na Karia kutokana na kauli zake walizodai kuwa zimewadhalilisha Wanayanga. "Sisi msimamo wetu ni kutokurudia mechi. Kwanza Rais wa TFF ametudhalilisha Wanayanga, na kama ameshindwa mpira, arudi kwenye taaluma yake, kwani tunaijua," wamesema kwa msisitizo. Kwa upande wake, Mratibu wa Yanga Dodoma, Elisha Ngwando, amemtaka Karia kuwaomba radhi Wanachama wa Yanga na wanamichezo kwa ujumla kwa maamuzi aliyofanya na kauli alizozitoa. "Watu wametumia gharama kubwa, wengine wamelipia matangazo kwa ajili ya mechi hiyo," amesema Ngwando. WanaYanga hao wameendelea kusisitiza kuwa hawataki mechi hiyo irudiwe, huku wakitoa wito kwa viongozi wa juu wa mpira nchini kuhakikisha haki inatendeka kwa klabu yao.

Jambo TV

29,653 ๆฌก่ง‚็œ‹ โ€ข 1 ๅนดๅ‰

VIDEO: Mbunge wa Jimbo la Ubungo na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo, amemjibu Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, John Heche, akisisitiza kuwa uongozi wa nchi unahitaji mipango na kura za wananchi badala ya maombi ya โ€˜kupewaโ€™ nchi ili kuijaribu. Akizungumza leo katika mkutano wa hadhara wa kuelezea utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) jimboni Ubungo mkoani Dar es Salaam kwa kipindi cha Novemba 2025 hadi Julai 2026, Prof. Kitila amerejea kauli ya Heche aliyoitoa hivi karibuni akidai kuwa upinzani ukipewa nchi kwa miaka miwili tu mabadiliko yataonekana. Prof. Kitila amefafanua kuwa katika mifumo ya kidemokrasia, uongozi haugawiwi kama zawadi bali unatafutwa kupitia ridhaa ya wananchi kwenye sanduku la kura. โ€œSasa kuna kiongozi mmoja wa upinzani nimemsikiliza juzi akiongea na vijana wa chama chao... anasema hivi sisi watupe nchi miaka miwili tu waone... Sasa unafikiri nchi unapewa? Huwa inapewa hivyo? Hii nchi uongozi unapatikana kwa kura sio kwa kupewa,โ€ amesema Prof. Kitila kwa msisitizo Prof. Kitila amebainisha kuwa uongozi ni dhamana nzito inayohitaji mikakati na siyo majaribio. Amesema kuwa CCM kimejikita katika mipango ya maendeleo wakati wapinzani wamebobea katika "kuzodoa". โ€œUongozi wa nchi sio uji kwamba kila mtu anataka apewa kuonja... uongozi wa nchi ni mipango, uongozi wa nchi ni mikakati. Uongozi wa nchi ni utawala bora... uongozi kuongoza sio kubobea kwenye kuzodoa. Wewe ukibobea kuzodoa, my friend, kuzodoa kupiga kelele nyingi hiyo inafurahisha,โ€ ameeleza Prof. Kitila Katika kulinganisha utendaji wa serikali ya CCM na nchi jirani, Prof. Kitila amebainisha kuwa Tanzania inatumia mikopo yake kwa ajili ya miradi ya kimkakati kama SGR, barabara na bandari, tofauti na mataifa mengine yanayokopa ili kulipa mishahara ya watumishi. Amesema hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa mipango ya maendeleo iliyoandaliwa na timu imara ya serikali.

Jambo TV

32,126 ๆฌก่ง‚็œ‹ โ€ข 21 ๅคฉๅ‰