Gerson Msigwa's banner
Gerson Msigwa's profile picture

Gerson Msigwa

@MsigwaGerson849,969 subscribers

The Permanent Secretary of Information, Culture, Arts and Sports || Chief Government Spokesperson of Tanzania.

Videos

MsigwaGerson's profile picture

TUHESHIMIANE.

Gerson Msigwa

148,259 views • 1 year ago

MsigwaGerson's profile picture

HATIMAYE meli yetu kongwe na ya kihistoria MV Liemba imeanza majaribio ikiwa ni maandalizi ya kuanza kazi rasmi ifikapo tarehe 01 Septemba, 2026 baada ya kusimama kwa takribani miaka 10 kutokana na kuhitaji ukarabati mkubwa. Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanikiwa kutafuna fupa gumu la kukarabati meli ili kuirejesha katika uhai mpya wa matumizi ya miaka 50. Kwa wasiojua meli hii ina umri wa miaka 113. Ilijengwa kwa mara ya kwanza nchini Ujerumani mwaka 1913 na Meyer Werft wa Papenburg, ikapewa jina la Graf von Goetzen ambaye alikuwa Gavana wa Kijerumani Afrika Mashariki. Kati ya mwaka 1914-1915 ilibomolewa katika vipande 5,000 ambavyo vilisafirishwa kwa meli mpaka Bandari ya Dar es Salaam na kisha kusafirishwa kwa treni kupitia reli ya kati (MGR) hadi katika fukwe za Ziwa Tanganyika Mkoani Kigoma ambako iliunganishwa upya kwa ajili ya kutumika katika Ziwa Tanganyika kusafirisha watu na mizigo. Wakati wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia, Ujerumani ilitawala Ziwa Tanganyika lakini kutokana na tishio kubwa la majeshi ya Wabelgiji na Waingereza, wafanyakazi Wajerumani wa meli hiyo waliamua kuizamisha majini katika Bandari ya Katabe ili kuificha isichukuliwe lakini kabla ya kuizamisha walipaka grisi katika injini yake yote ili isiharibiwe na maji. Hata hivyo, mwaka 1924 timu uokozi ya majeshi ya wanamaji wa Uingereza baada ya kukamata utawala iliibua meli hiyo kutoka katika sakafu ya Ziwa Tanganyika na mwaka 1927 Waingereza walifanikiwa kuirejesha katika matumizi ikisafirisha watu na mizigo. Wakati huo ndipo wakaibadilishwa jina na kuiita MV Liemba (Liemba ni neno la kabila la Kirungu likiwa na maana ziwa) Tangu wakati huo meli hii imekuwa katika matumizi mpaka mwaka 2016 ilipokuwa katika hali mbaya zaidi na hatimaye kusimamishwa kutokana na kuhitaji matengenezo makubwa. Serikali imefanya ukabari wa kufunga kila kitu kipya na cha kisasa. Sasa meli ina uwezo wa kubeba abiria 600 na tani 200 za mizigo ikiwa na kasi zaidi na mifumo yote mipya. Itatumika kuhudumia Tanzania, Zambia, Burundi na Kongo. Kwa ufupi tuna meli kwa biashara, usafiri wa watu na utalii. (Mzee NONGWA ole wako useme hili nalo halina maana🤣🤣)

Gerson Msigwa

14,394 views • 28 days ago