Peter Msigwa's banner
Peter Msigwa's profile picture

Peter Msigwa

@MsigwaPeter24,716 subscribers

Pastor | Former Member of parliament-iringa constituency 2010 -2020 | Former Shadow Minster for Natural Resource and Tourism 🇹🇿

Shorts

Yaani Mwamba amefikia level hizi Huku ni kushuka kisiasa kulikopitiliza 🤣🤣

Yaani Mwamba amefikia level hizi Huku ni kushuka kisiasa kulikopitiliza 🤣🤣

54,947 views

Hapa ni mwaka 1987 nikiwa muuza mitumba !sijui mwenzangu ulikuwa wapi mimi nilikuwa na hii Benz yangu. Najivunia Historia hii

Hapa ni mwaka 1987 nikiwa muuza mitumba !sijui mwenzangu ulikuwa wapi mimi nilikuwa na hii Benz yangu. Najivunia Historia hii

57,571 views

Kwa jirani mambo ni moto🤣🤣🤣🤣 wanaonyeshana makali

Kwa jirani mambo ni moto🤣🤣🤣🤣 wanaonyeshana makali

46,465 views

Watu wasio weza kujisimamia na kujiongoza wenyewe (CHADEMA) wanawezaje kuongoza Nchi. Wamevurugana kwa Rushwa za uchaguzi huko Njombe. Mmoja wa wagombea akiwatumia wapiga kura rushwa kwa simu yake mwenyewe! Hapa bado hamuelewi wapi?

Watu wasio weza kujisimamia na kujiongoza wenyewe (CHADEMA) wanawezaje kuongoza Nchi. Wamevurugana kwa Rushwa za uchaguzi huko Njombe. Mmoja wa wagombea akiwatumia wapiga kura rushwa kwa simu yake mwenyewe! Hapa bado hamuelewi wapi?

12,234 views

Videos

MsigwaPeter's profile picture

Kati ya mambo yaliyoniumiza sana nilipokuwa ugenini, moja kubwa lilikuwa ni wimbo wa “Aiyaiya CHADEMA.” Watu wengi hawajui kwamba wimbo huo niliutunga mimi mwenyewe. Mwanzoni haukuwa wimbo wa kitaifa wa chama; uliandaliwa mahsusi kwa ajili ya kampeni yangu ya ubunge wa Iringa Mjini mwaka 2020. Niliwaomba vijana wa kanisani kwangu wauimbe, na kwa pamoja tukaunda wimbo uliobeba matumaini na ari ya mabadiliko kwa wananchi wa Iringa. Sikutegemea hata kidogo kwamba ungependwa kwa kiwango kikubwa namna ile. Polepole ukaanza kuvuka mipaka ya jimbo letu. Baada ya Mheshimiwa Tundu Lissu kuteuliwa kuwa mgombea urais wa CHADEMA, baadhi ya viongozi na wanachama waliniomba niuongeze ubora wake ili uwe wimbo wa kitaifa, ukibeba majina ya Mwenyekiti wa chama wa wakati huo, mgombea urais na mgombea mwenza. Ndipo wimbo ukapata maisha mapya. Ukawa zaidi ya wimbo wa kampeni za Iringa Mjini; ukawa sehemu ya kumbukumbu na hisia za harakati za Watanzania wengi. Nilipokuwa upande mwingine wa kisiasa, kila nilipousikia wimbo huu, niliguswa sana. Haukuwa tu muziki; ulikuwa ukinikumbusha safari niliyopitia, watu tuliotembea pamoja, na ndoto tulizowahi kuziamini kwa moyo mmoja. Ilikuwa ni hisia ambazo ni vigumu kuzielezea kwa maneno. Leo ninafurahi kuona kwamba wimbo huu haujapoteza mvuto wake. Bado unaimbwa. Bado unawagusa watu. Bado unaishi mioyoni mwa wengi. Kwangu, hilo ni ukumbusho kwamba kazi inayofanywa kwa moyo wa kweli inaweza kuishi muda mrefu kuliko mazingira yaliyoiunda. Nilipoutunga ulikuwa wa Iringa Mjini. Leo umekuwa sehemu ya historia ya harakati za wengi. Na hilo ni jambo la kumshukuru Mungu.

Peter Msigwa

43,422 views • 1 month ago

MsigwaPeter's profile picture

MAFUTA SI MALI YA SERIKALI; NI MALI YA WATANZANIA. HIVYO, WATANZANIA WANA HAKI YA KUJUA. Mafuta ni bidhaa ya kimkakati. Bei yake huathiri gharama za usafiri, uzalishaji, kilimo, biashara na hatimaye maisha ya kila Mtanzania. Kwa sababu hiyo, mchakato wa uagizaji wa mafuta unapaswa kuwa wa uwazi, ushindani wa haki na uwajibikaji. Kwa maslahi ya umma, mamlaka husika zinapaswa kutoa majibu ya wazi kwa maswali yafuatayo: Ni kampuni gani imepewa zabuni ya kuingiza mafuta nchini kwa sasa? Zabuni hiyo ilitangazwa lini, ilitangazwa kwa utaratibu upi, na ni kampuni ngapi ziliwasilisha zabuni zao? Ni vigezo gani vya kitaalamu, kifedha na kisheria vilitumika kumchagua mshindi wa zabuni hiyo? Kampuni ya Namaro ni ya nani? Imesajiliwa katika nchi gani? Ina uzoefu gani katika biashara ya mafuta, na ilikidhi vipi masharti ya zabuni? Je, kuna uhusiano wowote wa kibiashara, kimiliki au wa kimkataba kati ya Namaro, Oilcom na Vitol? Ikiwa upo, ni wa aina gani? Mkataba huu utaongeza ushindani na kupunguza gharama za mafuta kwa wananchi, au utaongeza mkusanyiko wa nguvu za soko kwa kampuni chache? Serikali imechukua hatua gani kuhakikisha kwamba mchakato huu unazingatia sheria za manunuzi, sheria za ushindani na unalinda maslahi ya Taifa? Haya si maswali ya uadui. Haya ni maswali ya uwajibikaji. Serikali inayosimamia rasilimali za umma kwa uwazi haina sababu ya kuogopa kuyajibu. Wananchi wanapouliza kuhusu namna biashara ya mafuta inavyoendeshwa, hawafanyi hivyo kwa sababu wanapinga maendeleo. Wanafanya hivyo kwa sababu mafuta yanagusa maisha yao kila siku, na wanataka kujiridhisha kwamba maamuzi yote yanafanywa kwa uwazi, kwa ushindani wa haki na kwa manufaa ya Taifa. Uwazi hujenga imani. Ukimya hujenga mashaka.

Peter Msigwa

18,808 views • 1 month ago

MsigwaPeter's profile picture

Mayai kwa afya ya akili!

Peter Msigwa

71,323 views • 1 year ago

MsigwaPeter's profile picture

Tujikumbushe kidogo!

Peter Msigwa

60,434 views • 1 year ago

MsigwaPeter's profile picture

It is good to be home!

Peter Msigwa

11,266 views • 3 months ago

MsigwaPeter's profile picture

Katoro moja

Peter Msigwa

48,654 views • 2 years ago