
Peter Msigwa
@MsigwaPeter • 24,308 subscribers
Pastor | Former Member of parliament-iringa constituency 2010 -2020 | Former Shadow Minster for Natural Resource and Tourism 🇹🇿
Shorts
Videos

MAFUTA SI MALI YA SERIKALI; NI MALI YA WATANZANIA. HIVYO, WATANZANIA WANA HAKI YA KUJUA. Mafuta ni bidhaa ya kimkakati. Bei yake huathiri gharama za usafiri, uzalishaji, kilimo, biashara na hatimaye maisha ya kila Mtanzania. Kwa sababu hiyo, mchakato wa uagizaji wa mafuta unapaswa kuwa wa uwazi, ushindani wa haki na uwajibikaji. Kwa maslahi ya umma, mamlaka husika zinapaswa kutoa majibu ya wazi kwa maswali yafuatayo: Ni kampuni gani imepewa zabuni ya kuingiza mafuta nchini kwa sasa? Zabuni hiyo ilitangazwa lini, ilitangazwa kwa utaratibu upi, na ni kampuni ngapi ziliwasilisha zabuni zao? Ni vigezo gani vya kitaalamu, kifedha na kisheria vilitumika kumchagua mshindi wa zabuni hiyo? Kampuni ya Namaro ni ya nani? Imesajiliwa katika nchi gani? Ina uzoefu gani katika biashara ya mafuta, na ilikidhi vipi masharti ya zabuni? Je, kuna uhusiano wowote wa kibiashara, kimiliki au wa kimkataba kati ya Namaro, Oilcom na Vitol? Ikiwa upo, ni wa aina gani? Mkataba huu utaongeza ushindani na kupunguza gharama za mafuta kwa wananchi, au utaongeza mkusanyiko wa nguvu za soko kwa kampuni chache? Serikali imechukua hatua gani kuhakikisha kwamba mchakato huu unazingatia sheria za manunuzi, sheria za ushindani na unalinda maslahi ya Taifa? Haya si maswali ya uadui. Haya ni maswali ya uwajibikaji. Serikali inayosimamia rasilimali za umma kwa uwazi haina sababu ya kuogopa kuyajibu. Wananchi wanapouliza kuhusu namna biashara ya mafuta inavyoendeshwa, hawafanyi hivyo kwa sababu wanapinga maendeleo. Wanafanya hivyo kwa sababu mafuta yanagusa maisha yao kila siku, na wanataka kujiridhisha kwamba maamuzi yote yanafanywa kwa uwazi, kwa ushindani wa haki na kwa manufaa ya Taifa. Uwazi hujenga imani. Ukimya hujenga mashaka.
Peter Msigwa18,440 Aufrufe • vor 8 Tagen

Matukio ya viongozi wa serikali kuzomewa hadharani si jambo la kupuuzwa; ni kengele ya tahadhari inayopaswa kuwashtua wote walioko madarakani. Kama sababu zinazowafanya wananchi, hasa vijana, kufikia hatua ya kuonyesha hasira na kutoridhika hadharani hazitashughulikiwa kwa dhati, basi hakuna kiongozi anayepaswa kujidanganya kuwa yuko salama. Hilo linawahusu mawaziri, wabunge, na hata viongozi wa ngazi za juu zaidi. Hasira ya wananchi haijitokezi ghafla; hujengwa na muda mrefu wa kusikilizwa kwa masikio ya uongozi yaliyofungwa. Heshima ya viongozi haitokani na vyeo wala mamlaka pekee. Hujengwa kwa kusikiliza wananchi, kujibu malalamiko yao kwa vitendo, na kutatua changamoto zinazowakabili. Serikali inayopuuza dalili za wazi za kutoridhika inajichimbia shimo lenyewe na kuongeza pengo kati yake na wananchi. Hivyo, badala ya kujifanya hakuna kinachoendelea, viongozi wanapaswa kuchukulia ishara hizi kama onyo kali la kujitathmini upya, kurekebisha mwenendo wao, na kuimarisha uwajibikaji wa kweli kwa wananchi.
Peter Msigwa11,807 Aufrufe • vor 16 Tagen
5:53
Sensitive content
This media may contain sensitive content.

Natoa pole nyingi sana kwa Msaidizi wa Mheshimiwa Tundu Lissu, Ndugu Jumbe, kufuatia tukio baya na la kinyama lililomtokea. Huu si utamaduni wa Watanzania, wala si maadili yanayopaswa kupewa nafasi katika jamii yetu. Tofauti za kisiasa zisigeuke sababu ya chuki, vitisho, au mashambulizi dhidi ya watu. Taifa lenye afya ya kisiasa hujengwa juu ya ushindani wa hoja, heshima ya utu wa binadamu, na kulinda haki ya kila mtu kuwa salama bila kujali itikadi yake. Wananchi, wakati umefika wa sisi sote kupaza sauti na kukemea matukio ya aina hii bila kujali tofauti zetu za kisiasa. Ukimya mbele ya uovu unaweza kuupa nguvu uovu wenyewe. Namtakia Ndugu Jumbe uponaji wa haraka na nguvu katika kipindi hiki kigumu. Pia naomba vyombo husika vifanye uchunguzi wa haraka, wa haki, na wa uwazi ili wote waliohusika wakamatwe na kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.
Peter Msigwa24,253 Aufrufe • vor 2 Monaten

“Yeyote aliyeratibu tukio la mwamba , uwezo wake ni mdogo sana , badala ya kumjenga mwamba limemdhalilisha sana, limembomoa zaidi na kumfanya aonekane kituko katika jamii. Tukio lina matobo mengi sana story haiungu kabisa . Kwa maoni yangu ushauri wa familia yake ni wa Busara sana, huu wa akina Bon wanamuingiza chaka” Wapambe wake wanasema hawataki mabadiliko ndani ya chadema, ila wanataka waibadilishe CCM🤣🤣
Peter Msigwa75,979 Aufrufe • vor 1 Jahr

Yaani Mwamba amefikia level hizi Huku ni kushuka kisiasa kulikopitiliza 🤣🤣
Peter Msigwa54,947 Aufrufe • vor 1 Jahr
1:57
Sensitive content
This media may contain sensitive content.